Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 51:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Munisikilize, enyi munaojua mambo ya haki, ambao sheria zangu ziko ndani ya mioyo yenu. Musiogope mazarau ya watu, wala kufazaishwa na masimango yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 51:7
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sheria ya Mungu wake ni ndani ya moyo wake, naye hapiti pembeni katika mwenendo wake.


Halafu nikasema: “Ninakuja. Katika kitabu imeandikwa juu yangu.


Bwana wetu Yawe atakiangamiza kifo milele! Atayafuta machozi katika nyuso za watu wote na kuondoa haya ya watu wake katika dunia yote. Yawe amesema hivyo.


Maana Yawe ni mwamuzi wetu, yeye ni mutawala wetu; Yawe ni mufalme wetu, yeye ndiye anayetuokoa.


aliwaambia: “Mumwambie bwana wenu kwamba Yawe anasema hivi: Usiogope kwa sababu ya maneno uliyoyasikia, ambayo watumishi wa mufalme wa Asuria wameyasema kwa kunitusi.


Yawe anasema hivi: Munisikilize enyi munaotaka kukombolewa, ninyi munaonitafuta mimi Yawe. Muangalie jiwe mulilochongwa toka ndani yake, mulima mulimochimbuliwa.


Usiogope, hautapata haya tena. Usifazaike, hautazarauliwa tena. Utaisahau haya uliyopata katika ujana wako, wala hautakumbuka tena mazarau ya ujane wako.


Sasa basi, wewe Yeremia ujiweke tayari. Simama! Uende kuwaambia mambo yote ninayokuamuru. Usiwaogope, kusudi mimi nisikufanye kuwa mwoga mbele yao.


Lakini, ewe mwanadamu usiwaogope hao wala maneno yao; maana uko katikati ya michongoma na miiba, nawe unaikaa pamoja na nge; usiogope maneno yao wala usitishwe na nyuso zao, maana hao ni watu waasi.


Musiwaogope wale wanaoweza kuua tu mwili, lakini wasioweza kuua roho. Lakini zaidi mumwogope Mungu anayeweza kuharibu mwili pamoja na roho katika jehenamu.


“Heri ninyi, wakati watu wanapowatukana na kuwatesa na kuwasingizia kila namna ya ubaya kwa sababu yangu.


“Heri ninyi wakati watu wanapowachukia, wanapojitenga nanyi, wanapowatukana na kuchafua jina lenu kwa ajili ya Mwana wa Mutu!


Basi mitume wakatoka katika baraza, wakifurahi sana kwa sababu walistahili kuzarauliwa kwa kuteswa kwa ajili ya Yesu.


Inaonekana wazi kwamba ninyi ni barua iliyoandikwa na Kristo na kutumwa kwa njia ya utumishi wetu. Barua hii inaandikwa si kwa wino, lakini kwa Roho wa Mungu Mwenye Uzima. Barua hiyo haikuandikwa juu ya vibao vya mawe, lakini katika mioyo ya watu.


Muweke ndani ya moyo wenu maneno hayo ninayowaamuru leo


Kitu ninachotaka tu, ni kumujua Kristo na uwezo wa ufufuko wake na kushirikiana naye katika mateso yake, nako kufa kwangu kufanane na kufa kwake.


Bila shaka, ninahesabu mambo yote kuwa kihombo kwa ajili ya faida kubwa ya kujua Kristo Yesu Bwana wangu. Kwa ajili yake nimekubali kupoteza vyote, nikivihesabu kuwa kama mavi, kusudi nimupate Kristo


“Hili ndilo agano nitakalofanya nao nyuma ya siku zile. Ni Bwana wetu Mungu anayesema hivyo. Nitawawezesha kuchunga sheria zangu ndani ya mafikiri, nikiziandika ndani ya mioyo yao.”


Ninyi ni wenye heri kama watu wakiwatukana kwa ajili ya Kristo, kwa kuwa Roho wa utukufu, maana yake Roho wa Mungu anakaa ndani yenu.


Sasa, wapagani wanashangaa kuona ninyi hamushirikiani nao tena katika maisha ya ovyo ovyo; na kwa hiyo wanawasingizia ninyi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ