21 Basi, sikiliza, ewe Yerusalema unayeteseka; sikiliza wewe uliyelewa, lakini sio kwa divai.
Mukuwe wapumbafu na kupumbazika: mupofuke na kuwa vipofu! Mulewe lakini si kwa divai; mupepesuke lakini si kwa pombe.
Amuka, ewe Yerusalema! Amuka usimame wima! Yawe amekukunywesha kikombe cha kasirani yake, nawe umekikunywa mpaka tone la mwisho, mpaka ukayumbayumba.
Ewe Yerusalema, uliteseka, ulitaabishwa na kukosa wa kukufariji, lakini nitakujenga upya kwa mawe ya bei kali, misingi yako itakuwa ya mawe ya yakuti.
Kwa hasira yangu niliwaponda watu, niliwalewesha kwa kasirani yangu; damu yao niliimwanga chini.
Amenijaza taabu, akanishibisha uchungu.