Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 51:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Wewe umenisahau mimi Yawe Muumba wako, niliyezitandaza mbingu, na kuiweka misingi ya dunia! Kwa sababu ya kasirani ya yule anayekutesa, unaendelea kuogopa siku zote kwamba yuko tayari kukuangamiza! Lakini hasira yake itafikia wapi?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 51:13
56 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, muke wake Zeresi na warafiki zake wakamushauria hivi: “Kwa nini asitengenezewe muti wa kutundikia, wenye urefu wa metre makumi mbili na mbili? Kesho asubui, unaweza kuzungumuza na mufalme kusudi Mordekayi auawe juu yake, kisha uende ukule karamu na mufalme kwa furaha.” Wazo hilo lilimufurahisha Hamani, naye akatengeneza muti ule.


Naye, Hamani akauawa pale kwenye muti aliokuwa amemutayarishia Mordekayi. Basi, hasira ya mufalme ikapoa.


Unaweza kuzitandaza mbingu kama yeye hata zikuwe ngumu kama kioo cha shaba?


Yeye peke yake alitandaza mbingu, na kuyakanyaga mawimbi ya bahari.


Umejifunika mwangaza kama kanzu, umekunjua mbingu kama hema;


Lakini bila kukawia walisahau matendo yake, wakaacha kutegemea shauri lake.


wakati ulipoinuka kutimiza hukumu, kuwaokoa wote wanaoteswa katika dunia.


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe wa majeshi anasema hivi: Enyi watu wangu munaokaa Sayuni, musiwaogope Waasuria ambao wanawapiga kwa fimbo, wakiinua gongo zao juu yenu kama walivyofanya Wamisri.


utaimba wimbo huu wa kumuchekelea mufalme wa Babeli: Jinsi gani mutesaji alikomeshwa! Ukali wake umekomeshwa!


Wakimbizi wa Moabu waishi kwenu, mukuwe kimbilio lao mbali na mwangamizaji. Mutesaji atakapokuwa ametoweka, mateso yatakapokuwa yamekoma, na wagandamizaji kutoweka katika inchi.


Maana wewe Israeli umemusahau Mungu aliyekuokoa, haukukumbuka Jiwe lako la kufichamia. Kwa hiyo, hata mukipanda mimea ya Bali, na kuitakasa kwa mungu wa kigeni;


Ninyi hamujui bado? Hamujapata kusikia? Hamukuambiwa tangu mwanzo? Hamujafahamu mwanzo wa dunia?


Dunia iliumbwa na yule anayeikaa juu ya mbingu; kutoka huko wakaaji wa dunia ni kama mapanzi! Yeye ametandika mbingu kama pazia, na kuzikunjua kama hema la kuishi ndani yake.


Hivi ndivyo anavyosema Yawe aliyeumba mbingu na kuzitandika kama hema, aliyeifanya dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake, anayewapa watu wanaokaa ndani yake uzima, na kuwajalia uzima wote wanaoishi ndani yake:


Yawe aliyewaumba enyi watu wa Yakobo, yeye aliyewafanya enyi watu wa Israeli, anasema hivi: Musiogope, maana mimi nimewakomboa; nimewaita kwa jina lenu nanyi ni wangu.


Yawe, Mukombozi wako, aliyekuumba tangu katika tumbo, anasema hivi: Mimi ndiye Yawe niliyeumba vitu vyote. Mimi peke yangu nilizitandaza mbingu, niliiumba dunia kwa nguvu yangu mwenyewe!


Ni mimi niliyeifanya dunia, na kuumba mwanadamu anayeishi humo. Mikono yangu ndiyo iliyozitandaza mbingu, na kundi lote la nyota liko kwa amri yangu.


Hivi ndivyo anavyosema Yawe aliyeumba mbingu, ndiye Mungu aliyeipa dunia umbo na kuifanya na kuiimarisha. Hakuiumba kusudi ibaki ukiwa, lakini aliipa umbo kusudi iikaliwe na viumbe vyake: Mimi ni Yawe, wala hakuna mwingine.


Kwa mukono wangu niliuweka musingi wa dunia, mimi mwenyewe nilizitandaza mbingu. Nikiziita mbingu na dunia, zinasimama haraka mbele yangu.


Nitawasukuma watesaji wako wakule miili yao wenyewe; watalewa damu yao wenyewe kama divai. Halafu wanadamu wote watatambua kwamba mimi ni Yawe, Mwokozi wako, Mukombozi wako, Mwenye Nguvu wa Yakobo.


Utaimarishwa katika haki, mbali na kaoneo, nawe hautaogopa kitu; mbali na hofu, maana haitakukaribia.


Mulimwogopa na kutishwa na nani hata mukasema uongo, mukaacha kunikumbuka mimi na kuacha kabisa kufikiri juu yangu? Mimi sikuwaambia kitu kwa muda murefu; ndiyo maana labda mukaacha kuniheshimu!


Umwambie akuwe macho, atulie na asiogope wala asivunjike moyo, kwa sababu ya hasira kali ya mufalme Resini wa Aramu, na ya mwana wa Remalia. Hao wawili ni kama tu moshi wa kuni zinazozimika.


Viatu vyote vya washambulizi katika vita na nguo zote zenye kujaa damu vitateketezwa kama kuni za kuwasha moto.


Kijana binti anaweza kusahau mapambo yake, au bibi arusi nguo yake? Lakini watu wangu wamenisahau kwa muda wa siku zisizohesabika.


Mufalme Zedekia akamwambia Yeremia: Ninawaogopa Wayuda waliokimbilia kwa Wakaldea. Labda nitatolewa kwao, wanitese.


walikuwa wanawaogopa Wakaldea tangu wakati Isimaeli mwana wa Netania, alipomwua Gedalia mwana wa Ahikamu ambaye mufalme wa Babeli alikuwa amemusimika kuwa mutawala wa inchi.


Yawe ndiye aliyeumba dunia kwa nguvu zake, aliyeuimarisha ulimwengu kwa hekima yake, na kwa akili yake akazitandaza mbingu.


Mungu anayekuwa hazina ya Yakobo si kama hizo, maana yeye ndiye aliyeviumba vitu vyote, na Israeli ni kabila linalokuwa mali yake; Yawe wa majeshi, ndilo jina lake.


Basi, mutakaposikia tena sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, muko tayari kuinama chini na kuiabudu sanamu niliyotengeneza? Kama mukikataa, mutatupwa mara moja katika furu la moto mukali. Ni mungu gani anayeweza kuwaokoa katika mikono yangu?


Lakini, hata kama haitafanyika hivyo, ujue wazi, ee mufalme, kwamba sisi hatutaitumikia miungu yako wala kuiabudu sanamu ya zahabu uliyosimamisha.


Kwa hiyo, mufalme Nebukadneza akawaka hasira, sura yake ikabadilika kwa chuki juu ya Sadiraki, Mesaki na Abedenego. Akaamuru kwamba moto wa furu uongezwe mara saba kuliko kawaida yake.


Na pale pale malaika wa Bwana akamwazibu Herode kwa ugonjwa kwa sababu alijitukuza kwa pahali pa Mungu. Herode akakuliwa na michango ya tumbo na kisha akakufa.


Basi, tuseme nini juu ya wenye hekima, walimu wa Sheria, nao wafundi wa usemi siku hizi? Mungu ameonyesha wazi kwamba hekima ya dunia hii ni upumbafu!


“Ewe kifo, ushindi wako uko wapi? Ewe kifo, uwezo wako wa kuua uko wapi?”


Hamukumujali Mulima wenu, yule aliyewapa uzima. Mulimusahau Mungu aliyewazaa ninyi.


muhakikishe kwamba hamutamusahau Yawe aliyewatoa Misri ambako mulikuwa watumwa.


“Muhakikishe kwamba hamutamusahau Yawe, Mungu wenu, kwa kutoshika amri zake, maagizo yake na masharti yake ninayowaamuru leo.


Kama wangekumbuka inchi yao walioiacha zamani, wangeweza kupata namna ya kurudia kule.


Yule nyama akakamatwa pamoja na yule nabii wa uongo aliyeonyesha vitambulisho mbele yake. (Ni kwa njia ya vitambulisho vile aliwadanganya wale waliopigwa chapa ya yule nyama na wale walioabudu sanamu yake.) Nyama yule pamoja na nabii wa uongo wakatupwa wangali wazima katika ziwa la moto munamowaka mawe ya kiberiti.


Walitawanyika katika dunia yote, na kuzunguka kambi ya watu wa Mungu na muji wake alioupenda. Lakini moto ukashuka toka mbinguni, ukawateketeza.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ