Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 51:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Yawe anasema hivi: Mimi, kweli mimi, ndiye ninayekufariji. Kwa nini wewe unamwogopa mutu ambaye ni wa kufa, mwanadamu ambaye anatoweka kama majani?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 51:12
37 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Malaika wa Yawe akamwambia Elia: “Shuka pamoja naye, wala usimwogope.” Basi, Elia akasimama, akashuka pamoja naye mpaka kwa mufalme.


Yawe yuko nami, siogopi kitu; mwanadamu ataweza kunifanya nini?


Mwanadamu akitoa pumzi yake ya mwisho, anarudi katika mavumbi alimotoka, na hapo mipango yake yote inatoweka.


Mutu mupumbafu hawezi kufahamu, wala mujinga hajui jambo hili:


Wengi wanapenda kujipendekeza kwa mutawala, lakini mutu anapata haki yake kwa Yawe.


Mungu ndiye mwenye kuniokoa, nitamutegemea yeye, wala sitaogopa; Yawe ananijalia nguvu; yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa.


Usimutumainie mwanadamu, uzima wake ni kama pumzi tu. Yeye anafaa kitu gani?


Mungu wenu anasema hivi: Muwafariji watu wangu. Muende kuwafariji.


Lakini mimi ndiye niliyefuta makosa yenu kwa heshima yangu, ndiye ninayefuta makosa kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka zambi zenu.


Muimbe kwa furaha, enyi mbingu! Ushangilie ewe dunia, Enyi milima, mulalamike kwa furaha, maana Yawe amewafariji watu wake, anawaonea huruma watu wake wanaoteseka.


Mimi Yawe nitaufariji Sayuni, nitatengeneza pahali pake pote palipoharibika. Nitazifanya mbuga zake kama shamba la Edeni, jangwa yake kama bustani ya Yawe. Ndani yake kutapatikana furaha na shangwe, na nyimbo za shukrani zitasikilika humo.


Mupige kelele za shangwe, enyi mabomoko ya Yerusalema! Yawe amewafariji watu wake, ameukomboa Yerusalema.


Mulimwogopa na kutishwa na nani hata mukasema uongo, mukaacha kunikumbuka mimi na kuacha kabisa kufikiri juu yangu? Mimi sikuwaambia kitu kwa muda murefu; ndiyo maana labda mukaacha kuniheshimu!


Amenituma kutangaza mwaka wake wa neema, na siku ya Mungu wetu ya kulipiza kisasi kusudi niwafariji wote wanaoomboleza.


Kama vile mama anavyomufariji mwana wake, vilevile nami nitawafariji; mutafarijiwa katika Yerusalema.


Musijiunge nao katika mashauri yao mabaya, wala musiogope yale wanayoyaogopa wala kuwa na hofu.


Mufalme Zedekia akamwambia Yeremia: Ninawaogopa Wayuda waliokimbilia kwa Wakaldea. Labda nitatolewa kwao, wanitese.


walikuwa wanawaogopa Wakaldea tangu wakati Isimaeli mwana wa Netania, alipomwua Gedalia mwana wa Ahikamu ambaye mufalme wa Babeli alikuwa amemusimika kuwa mutawala wa inchi.


Lakini, ewe mwanadamu usiwaogope hao wala maneno yao; maana uko katikati ya michongoma na miiba, nawe unaikaa pamoja na nge; usiogope maneno yao wala usitishwe na nyuso zao, maana hao ni watu waasi.


Musiwaogope wale wanaoweza kuua tu mwili, lakini wasioweza kuua roho. Lakini zaidi mumwogope Mungu anayeweza kuharibu mwili pamoja na roho katika jehenamu.


“Sitawaacha kama wayatima, nitawarudilia tena.


Wakati ule, kanisa lilikuwa na amani katika Yudea yote, Galilaya na Samaria. Vilevile lilizidi kupata nguvu na kuendelea kumwogopa Bwana, nalo liliongezeka kwa musaada wa Roho Mutakatifu.


Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Wanadamu wote ni kama majani. Na utukufu wao wote unatoweka kama maua. Majani yanakauka na maua yanaanguka.


Saulo akamwambia Samweli: “Nimetenda zambi. Nimeasi amri ya Yawe na amri yako, kwa sababu niliwaogopa watu, nikawatii wao.


Saulo pamoja na waaskari wote wa Israeli walipoyasikia maneno hayo ya Mufilistini yule, walifazaika na kuogopa sana.


Daudi akafikiri sana juu ya maneno yale, akaanza kumwogopa sana Akisi mufalme wa Gati.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ