Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 50:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Bwana wetu Yawe amenifundisha jinsi ya kusema, kusudi niwatie moyo wale waliochoka. Kila asubui ananipa hamu ya kusikiliza mambo anayotaka kunifundisha.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 50:4
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Maneno yako yamewainua moyo, umewaimarisha waliokosa nguvu.


Ninaamuka mbele ya mapambazuko na kukuomba musaada; ninaweka tumaini langu katika maneno yako.


Kila asubui unionyeshe wema wako, maana ninakutumainia. Unifundishe mwenendo wa kufuata, maana ninakutolea moyo wangu.


Wewe hautaki sadaka za kuteketezwa kwa moto wala matoleo, sadaka za nyama za kuteketezwa wala za kusamehewa zambi, lakini umenipa masikio nikusikie.


Moyo wangu umejaa mawazo mazuri: ninamutungia mufalme mashairi yangu, ulimi wangu ni kama kalamu ya mwandishi hodari.


Usikilize kilio changu, Mufalme wangu na Mungu wangu, maana wewe ndiwe ninayekuomba.


Maajabu yako yanajulikana humo katika giza, au matendo yako ya haki katika inchi ya waliosahauliwa?


Wasiwasi ndani ya moyo inamukosesha mutu raha, lakini neno zuri linamuchangamusha.


Kutoa jibu zuri kunafurahisha; neno linalofaa kwa wakati wake ni jema sana!


Neno linalosemwa kwa wakati unaofaa, ni kama michoro ya zahabu juu ya feza.


Kila mara itakapopita kwenu itawapata; nayo itapita kila asubui, muchana na usiku. Kusikia ujumbe huu tu kutakuwa kitisho.


Wao wananichekelea na kuuliza: Huyu nabii anataka kufundisha nani? Anazani atatuelezea sisi ujumbe wake? Sisi ni watoto wachanga walioachishwa kunyonya juzijuzi?


Hapo vipofu wataona tena, na viziwi watasikia tena.


Yeye anawapatia nguvu wanaokuwa zaifu, anawaongezea nguvu wale wanaoregea.


Nani kati yenu anayemwogopa Yawe? Nani anayetii maneno ya mutumishi wake? Kama kuna mutu anayetembea katika giza bila taa, amutumainie Yawe, na kumutegemea Mungu wake.


Watu wako watafundishwa nami Yawe, wana wako watapata ustawi mwingi.


Nitalinda agizo hilo na kuchunga mafundisho hayo kati ya wafuasi wangu.


Kisha Yawe akanyoosha mukono wake, akagusa kinywa changu, akaniambia: Nimetia maneno yangu ndani ya kinywa chako.


Waliochoka nitawachangamusha, na waregevu nitawapa nguvu.


Kila siku asubui mutamutolea Yawe mwana-kondoo wa mwaka mumoja asiyekuwa na kilema, ambaye atateketezwa kwa moto.


“Mukuje kwangu ninyi wote munaosumbuka na kulemewa na mizigo mizito, nami nitawapumzisha.


na kwenda katika muji wake mwenyewe. Kule akaanza kuwafundisha watu katika nyumba zao za kuabudia, nao walishangaa na kuuliza: “Huyu amepata hekima na miujiza hii kutoka wapi?


Basi hakuna mutu aliyeweza kumujibu neno, na tangia siku ile hakuna aliyesubutu kumwuliza tena neno.


Kwa maana mimi mwenyewe nitawapa masemi na hekima hata waadui zenu hawataweza kuyapinga wala kuyakataa.


Nao wote wakamufurahia na kushangaa na maneno mazuri aliyosema. Wakasema: “Huyu si mwana wa Yosefu?”


Walinzi wakajibu: “Hatujasikia mutu akisema sawasawa na mutu yule!”


Nitawachagulia kati ya wandugu zao wenyewe nabii kama wewe, nitatia maneno yangu ndani ya kinywa chake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ