Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 5:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Ole kwao wanaoongeza nyumba juu ya nyumba, wanaoongeza mashamba juu ya mashamba yao, mpaka kila sehemu inakuwa mali yao, na hakuna nafasi kwa wengine katika inchi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 5:8
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ameishi katika miji iliyoachwa wazi, katika nyumba zisizokaliwa na mutu, nyumba zilizotakiwa zikuwe lundo la uharibifu.


Kisha kula hakuacha hata makombo. Kwa hiyo fanaka yake yote haitadumu.


Anayetamani faida ya unyanganyi anataabisha jamaa yake, lakini anayechukia kituliro ataishi.


Wewe mwanadamu, wandugu zako na wakaaji wa Yerusalema ambao vilevile ni wandugu zako wanasema juu yako na juu ya watu wote wa Israeli wanaokuwa katika uhamisho hivi: Ninyi munaokuwa katika uhamisho muko mbali sana na Yawe; maana Yawe ametupatia sisi inchi hii ikuwe mali yetu.


Wewe mwanadamu! Wakaaji waliobaki katika miji iliyoharibiwa katika inchi ya Israeli wanasema: Abrahamu alikuwa peke yake, hata hivyo, alipata kurizi inchi hii. Lakini sisi ni wengi; ni wazi tumepewa inchi hii ikuwe yetu!


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Amoni, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Katika vita yao kwa kupanua inchi, walipasua tumbo za wanawake wenye mimba katika inchi ya Gileadi.


Ole wao wanaopanga kutenda maovu, wanaolala usiku wakikusudia mabaya! Mara tu kunapopambazuka, wanayatimiza maana wako na uwezo.


Wanatamani mashamba na kuyatwaa; wakitaka nyumba, wananyanganya. Wanawatesa wenye nyumba na jamaa zao, wanawanyanganya watu mali zao.


Kila mutu atamuchekelea mutu wa namna hiyo na kumutungia misemo ya kitambi: Ole wako unayejilundikia visivyokuwa vyako, na kutwaa rehani mali za watu lakini haulipi! Utaendelea kufanya hivyo mpaka wakati gani?


“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munawafungia watu wengine njia ya kuingia katika Ufalme wa mbinguni. Ninyi wenyewe hamwingii mule na zaidi ya hii munawazuiza wale wanaotaka kuingia. [


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ