Isaya 5:30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
30 Siku hiyo, watanguruma juu ya Israeli kama uvumi wa bahari iliyochafuka. Atakayeiangalia inchi kavu ataona giza tupu na taabu, mwangaza utafunikwa na mawingu.
Musikilize kelele kwenye milima kama za kundi kubwa la watu! Musikilize kelele za falme, na mataifa yanayokusanyika! Yawe wa majeshi analichunguza kundi linalokwenda kwa vita.
Ujumbe wa Mungu juu ya nyama wa pande za jangwa ya kusini: Wajumbe wanapita katika inchi ya taabu na shida, yenye simba, nyoka wa sumu na nyoka wakubwa wanaoruka. Wamewabebesha punda na ngamia wao mali zao, kuwapelekea watu wasioweza kuwafalia kitu.
Kwa hiyo, kufuata sheria ya Mungu kuko mbali nasi, haki haifiki kwetu. Tulitazamia kupata mwangaza, kumbe ni giza tupu; tulingojea mwangaza, lakini tunatembea katika giza.
Mumutukuze Yawe, Mungu wenu, mbele hajawaletea giza, mbele hamujajikwaa miguu kwenye milima inayofunikwa na giza. Ninyi mulitazamia mwangaza, lakini anaugeuza kuwa usiku anaufanya kuwa giza nzito.
Wameshika pinde zao na mikuki; ni watu wakali wasiokuwa na huruma. Vishindo vyao ni kama uvumi wa bahari, wamepanda juu ya farasi. Wamejipanga tayari kwa vita na wewe Babeli!
Wameshika pinde zao na mikuki; ni watu wakali wasiokuwa na huruma. Vishindo vyao ni kama uvumi wa bahari. Wamepanda juu ya farasi, wamejipanga tayari kwa vita na wewe Sayuni!
“Mara moja kisha mateso ya siku zile, jua litatiwa giza, mwezi hautaangaza, nyota zitaanguka toka mbinguni na vyote vyenye nguvu katika mbingu vitatikiswa.
Kisha nikaona mambo haya: Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa sita, kukakuwa tetemeko kubwa la dunia; jua ikageuka kuwa nyeusi kama nguo ya kilio na mwezi ukageuka kuwa mwekundu kama damu.