Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 5:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

29 Waaskari wao wananguruma kama simba; wananguruma kama simba wakali ambao wamekamata nyama wao na kuwapeleka mbali ambapo hakuna anayeweza kuwanyanganya.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 5:29
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wewe Yuda, mwana wangu, ni kama mwana-simba ambaye amepata mawindo yake akapanda juu, kama simba mukali anajinyoosha na kulala chini. Simba dike, nani anayesubutu kumwamusha?


“Mufikiri vizuri jambo hili, enyi musionijali, kama sivyo nitawaangamiza, wala hakuna atakayewaokoa.


Nilimutuma kuliazibu taifa ovu, nilimwamuru kuwaazibu watu niliowakasirikia, kuwanyanganya na kuteka vitu vyao, na kuwakanyaga chini kama matope katika njia.


Yawe aliniambia hivi: Simba mukali ananguruma kwa kukinga nyama aliyemukamata; hata kundi la wachungaji likiitwa kwa kumufukuza, hatishiki kwa kelele zao, wala hashituki kwa sauti zao. Ni vile Yawe wa majeshi atakavyoshuka kupigana juu ya mulima Sayuni na kilima chake.


humo hamutakuwa simba, nyama yeyote mukali hatapitia humo, hao hawatapatikana humo. Lakini waliokombolewa ndio watakaopita humo.


Lakini hawa ni watu walioibwa mali yao na kunyanganywa! Wote wamenaswa katika mashimo, wamefungwa katika kifungo. Wamenyanganywa bila mutu wa kuwaokoa, wamekamatwa mateka na hakuna anayesema: Muwarudishe!


Ndivyo watakavyokuwa hao uliowategemea hivyo, hao uliojishugulisha nao tangu ujana wako. Watatangatanga kila mumoja njia yake; hakuna hata mumoja atakayeweza kukuokoa.


Simba wananguruma kwa ajili yake, wananguruma kwa sauti kubwa. Wameiharibu kabisa inchi yake, miji yake imebaki mabomoko pasipo watu.


Kama simba anavyotoka kwenye maficho yake, mwangamizaji wa mataifa ameanza kuja, anakuja kutoka pahali pake, kusudi aharibu inchi yenu. Miji yenu itabaki mabomoko matupu, bila kukaliwa na mutu yeyote.


Kama vile simba anavyochomoka kutoka ndani ya vichaka vya muto Yordani na kuingia kwenye mbuga, ndivyo nitakavyowafukuza kwa rafla Waedomu toka katika inchi yao. Nami nitamuweka huko mutawala yeyote nitakayemuchagua. Maana, ni nani anayeweza kulinganishwa nami? Nani anayeweza kunishitaki? Ni muchungaji gani anayeweza kunipinga?


Israeli ni kama kondoo wanaowindwa na kufukuzwa na simba. Kwanza waliangamizwa na mufalme wa Asuria, na sasa Nebukadneza mufalme wa Babeli, amevunjavunja mifupa yake.


Wababeli watanguruma pamoja kama simba; watalia kama wana-simba.


Watanifuata mimi Yawe ninayenguruma kama simba; nitakaponguruma watanifikia toka magaribi wakitetemeka.


Simba akinguruma, ni nani asiyeogopa? Bwana wetu Yawe akisema, ni nani atakataa kuutangaza ujumbe wake?


Waisraeli watawashinda waadui zao na kuwaangamiza kabisa.


Muji wa Ninawe ni maangamizi matupu na uharibifu! Watu wamekufa moyo, magoti yanagongana, nguvu zimewaishia, nyuso zimebadilika!


Wakubwa wake ni simba wanaonguruma, waamuzi wake ni imbwa wa pori wenye njaa magaribi wasioacha chochote mpaka asubui.


Sikia maombolezo ya watawala! Utukufu wao umeharibiwa! Sikia ngurumo za simba! Pori la muto Yordani limeharibiwa!


Atavizia na kulala chini kama simba, nani atasubutu kumwamusha? Abarikiwe yeyote atakayekubariki wewe Israeli, alaaniwe yeyote atakayekulaani.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ