Naye atasimika bendera kuwaita mataifa, kuwakusanya Waisraeli waliozarauliwa, kuwaleta pamoja watu wa Yuda waliotawanywa, na kuwarudisha toka pembe ine za dunia.
Mungu anasema: Musimike bendera juu ya mulima usiokuwa na miti, muwapigie waaskari kelele, muwapepee watu kwa mukono, mukiwaita waingie kwenye milango ya muji wa wakubwa.
Musikilize kelele kwenye milima kama za kundi kubwa la watu! Musikilize kelele za falme, na mataifa yanayokusanyika! Yawe wa majeshi analichunguza kundi linalokwenda kwa vita.
Pahali pake mulisema: Hapana! Sisi tutakimbia na farasi wenye mbio. Sawa, mutakimbia na farasi wenye mbio, lakini farasi wa waadui zenu wana mbio zaidi.
Mufalme wao atatoroka kwa ajili ya hofu, na wakubwa wao wataiacha bendera yao kwa ajili ya woga. –Ni ujumbe wa Yawe ambaye moto wake uko katika Sayuni, ambaye furu lake liko katika Yerusalema.
Halafu nabii Isaya alikwenda kwa mufalme Hezekia na kumwuliza: Watu hawa wamesema nini? Na wametoka wapi? Naye Hezekia akamujibu: Wamekuja kutoka inchi ya mbali, kule Babeli.
Angalia! Adui anakuja akivuma kama mawingu. Magari yake ya vita ni kama zoruba, nao farasi wake wa vita wanaruka mbio kuliko tai. Ole kwetu! Tumeangamia!
Na kwa ngambo yenu ninyi watu wa Israeli, ninaleta taifa moja kutoka mbali kuwashambulia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Hili taifa haliwezi kushindwa, ni taifa la zamani, ni taifa ambalo hamufahamu luga yake. Hamuwezi kuelewa hata neno wanalolisema.
Pandisha bendera ya vita katika dunia, piga baragumu kati ya mataifa; uyatayarishe mataifa kwa kupigana naye; uziite falme kwa kuishambulia; falme za Ararati, Mini na Askenazi. Weka jemadari juu yake; ulete farasi kama makundi ya nzige.
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Wewe ndiwe niliyesema habari zako hapo zamani kwa njia ya watumishi wangu manabii wa Israeli, ambao walitabiri nyakati zile kwamba nitakuleta kusudi ushambulie watu wa Israeli.
Farasi wao ni wepesi kuliko chui, wakali kuliko imbwa wa pori wenye njaa. Waaskari wapanda-farasi wao wanatoka mbali, wanaruka mbio kama tai anavyorukia nyama.
Watu wa mataifa katika dunia yote tokea upande jua linapopanda mpaka upande jua linaposhuka wanalitukuza jina langu. Kila pahali wananifukizia ubani na kunitolea sadaka zinazokubaliwa; maana jina langu linatukuzwa kati yao.