Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 5:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Kwa hiyo hasira ya Yawe iliwawakia watu wake, akaunyoosha mukono wake juu yao, akawaazibu. Milima ikatetemeka, maiti zao zikakuwa kama takataka katika barabara za muji. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 5:25
60 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mutu yeyote wa jamaa ya Yeroboamu atakayekufia katika muji, imbwa watamukula; na yeyote atakayekufia katika shamba, ndege watamukula.’ Yawe amesema hivyo.”


Mutu yeyote wa jamaa yako atakayekufia ndani ya muji, imbwa watamukula; na mutu yeyote atakayekufia katika shamba, ndege watamukula.”


Hakika, mutu yeyote wa jamaa yake atakayekufia ndani ya muji, imbwa watamukula; na mutu yeyote atakayekufia katika shamba, ndege watamukula.’ ”


Yawe alikasirika, akawafanya watu wa Israeli washindwe katika vita mara kwa mara na mufalme Hazaeli wa Aramu na mwana wake Beni-Hadadi.


Maiti ya Yezebeli itakuwa kama mboleo ndani ya shamba katika inchi ya Yezereheli, hata hakuna atakayeweza kumutambua.’ ”


Lakini wao waliendelea kuwachekelea wajumbe wa Mungu, wakayazarau maneno yake na kuwachekelea manabii wake mpaka kwa mwisho kasirani ya Yawe ikawaka juu ya watu wake hata hakukukuwa wa kuwaponyesha.


Mungu hatazuia hasira yake; Rahabu na wasaidizi wake wanainama chini mbele yake.


Hasira ya Yawe ikawawakia watu wake, akachukizwa sana na hao waliokuwa mali yake.


Utetemeke, ee dunia, mbele ya Yawe; utetemeke mbele ya Mungu wa Yakobo,


Katika taabu yangu, nilimwita Yawe; nilimulilia Mungu wangu anisaidie. Toka katika hekalu lake, alisikia sauti yangu; kilio changu kilimufikia katika masikio yake.


Ee Mungu, ulipowaongoza watu wako, uliposafiri kule katika jangwa,


Mawingu yalinyesha mvua nyingi, ngurumo zikavuma katika anga, mishale ya umeme ikaangaza kila upande.


Lakini Mungu mwenye huruma alisamehe uovu wao, wala hakuwaangamiza. Mara nyingi alizuia hasira yake, wala hakuacha kasirani yake yote iwake.


Uwatendee ulivyowatendea Wamidiani, ulivyowatendea Sisera na Mufalme Asikie kwenye muto Kisoni,


Yawe akamwambia Musa: “Umwambie Haruni atwae fimbo yake na kuiinua juu ya maji ya Misri, juu ya mito yote, mifereji, visima na maji yao yote, nayo yatakuwa damu. Kutakuwa damu katika inchi yote, na hata katika vyombo vyote vya muti na vya mawe.”


Hakuna! Mutajikunja tu kati ya wafungwa na kuangamia pamoja na wanaouawa katika vita. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Nilimutuma kuliazibu taifa ovu, nilimwamuru kuwaazibu watu niliowakasirikia, kuwanyanganya na kuteka vitu vyao, na kuwakanyaga chini kama matope katika njia.


Lakini wewe umetupwa inje ya kaburi lako, kama mutoto wa kuchukiza aliyezaliwa mufu, kama maiti ambayo imekanyagwakanyagwa. Umelundikiwa maiti za waliouawa kwa upanga, waliotupwa ndani ya mashimo penye mawe.


Yawe ameunyoosha mukono wake juu ya bahari amezitetemesha falme; ametoa amri kuharibu makimbilio ya Kanana.


Watainyoosha mikono yao kama mutu anayejaribu kuogelea, lakini pamoja na bidii yao, Yawe ataporomosha kiburi chao.


lakini mimi Mungu nitahuzunisha Yerusalema, ndani yake kutakuwa vilio na maombolezo, muji wenyewe utakuwa kama mazabahu.


Kwa hiyo aliwamwangia kasirani yake kali, akawaacha kupatwa na vita kali. Hasira yake iliwawakia kila upande, lakini wao hawakuelewa chochote; iliwachoma, lakini hawakufikiri juu ya jambo hilo.


Watoto wako wamezimia, wamelala pembeni ya kila barabara, wako kama paa aliyenaswa ndani ya mutego. Wamepatwa na kasirani ya Yawe, wamepatwa na azabu ya Mungu wako.


Tangu zamani hakuna aliyepata kusikia kwa masikio yake wala kumwona Mungu anayekuwa kama wewe, anayetenda mambo kama hayo kwa ajili ya wale wanaomutegemea!


Yawe atakuja kama moto, na magari yake ya vita ni kama zoruba. Ataiacha hasira yake ifanye kazi yake kwa ukali, na maonyo yake yatimizwe kwa ndimi za moto.


Kisha watakwenda kuziona maiti za wale walioniasi. Wadudu watakaowakula hawatakufa, na moto utakaowachoma hautazimika hata kidogo. Watakuwa chukizo kwa watu wote.


Waasuria kwa upande wa mashariki, Wafilistini kwa upande wa magaribi, wamepanua vinywa vyao kwa kuimeza Israeli. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Kwa hiyo, Yawe hawahurumii vijana wao, hana huruma juu ya wayatima na wajane wao; maana hakuna hata mumoja anayemufuata, kila mutu anasema upumbafu. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Uovu unawaka kama moto unaoteketeza michongoma na miiba; unawaka kama moto katika pori, na kutoa moshi muzito unaopanda juu katika anga.


Manase anashambulia Efuraimu, Efuraimu anashambulia Manase na wote wawili wanashambulia Yuda. Hata hivyo, hasira ya Yawe haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Nimeamua kuleta aina ine za maangamizi juu yao: upanga kwa kuwaua, imbwa kwa kuwararua, ndege na nyama wa pori kwa kuwakula na kuwamaliza.


Hao watakufa kwa magonjwa makali, na hakuna atakayeomboleza juu yao wala kuwazika. Maiti zao zitabaki kama vile mboleo juu ya udongo. Wataangamia kwa vita na kwa njaa; na maiti zao zitakuwa chakula cha ndege na nyama wa pori.


Itawabidi kuiacha hiyo inchi yenu niliyowapa, nami nitawafanya muwatumikie waadui zenu katika inchi musiyoijua, kwa sababu hasira yangu imewaka kama moto usiozimika hata milele.


Niliangalia milima, nikaiona ikitetemeka, navyo vilima vyote vilikuwa vikiyumbayumba.


Kwa hiyo, muvae gunia, muomboleze na kulia; kwa maana Yawe hajaondoa hasira yake kali kwenu.


Nyumba zao zitapewa watu wengine, nayo mashamba yao na wake zao vilevile; maana nitaunyoosha mukono wangu, kuwaazibu wakaaji wa inchi hii. –Ni ujumbe wa Yawe.


Itaachwa imetandazwa mbele ya jua na mwezi na nyota zote za mbingu, vitu ambavyo walivyopenda na kuvitumikia, na kuviendea kwa kuuliza shauri na kuviabudu. Mifupa hiyo haitakusanywa wala kuzikwa, lakini itabaki kama vile mboleo juu ya udongo.


Yawe anasema hivi: Mwenye hekima asijivunie hekima yake, mwenye nguvu asijivunie nguvu yake; wala tajiri asijivunie utajiri wake.


Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kama vile nilivyoutoa muti wa muzabibu kati ya miti ya pori kuwa kuni za kukonga moto, ndivyo nilivyotoa wakaaji wa Yerusalema.


Nitaimarisha mikono ya Mufalme wa Babeli, lakini mikono ya Mufalme wa Misri itaregea. Hapo watu watatambua kwamba mimi ni Yawe. Nitakapotia upanga wangu katika mukono wa Mufalme wa Babeli, ataunyoosha juu ya inchi ya Misri kwa kuiazibu,


Nitanyoosha mukono wangu juu yao, na kuiharibu inchi yao. Tangu huko katika jangwa upande wa kusini mpaka katika muji wa Dibla kwa upande wa kaskazini, nitaifanya inchi yao kuwa matongo kabisa wasipate pahali pa kuishi. Nao watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Ee Bwana, kwa kadiri ya matendo yako ya haki usiukasirikie wala kuwa na hasira kwa ajili ya muji wako Yerusalema, mulima wako mutakatifu. Watu wote wa inchi za jirani wanauzarau Yerusalema na watu wako, kwa sababu ya zambi zetu na maovu babu zetu waliyotenda.


Inchi ya Asuria haitatuokoa, hatutategemea tena farasi wa vita. Hatutaziita tena Mungu wetu hizo sanamu tulizochonga. Kwako, ee Mungu, yatima anapata huruma.


Kwa hiyo, dunia itatetemeka na kila mutu katika inchi atafanya kilio. Inchi yote itayumbayumba; itapanda na kushuka, kama vile maji ya muto Nili yanavyojaa na kupunguka!


Milima itayeyuka chini ya miguu yake, kama inta karibu na moto; mabonde yatapasuka, kama vile maji yanayoporomoka kwenye muteremuko.


Milima inatetemeka mbele yake, vilima vinayeyuka. Dunia inatetemeka mbele yake, ulimwengu na vyote vinavyokuwa ndani yake.


Milima ilikuona, ikanyauka; mafuriko ya maji yakapita mule. Vilindi vya bahari vilinguruma, na kurusha juu mawimbi yake.


Kwa maana watu wamemukosea Yawe, yeye atawaletea taabu kubwa, wao watatembea kama vipofu. Damu yao itamwangwa kama mavumbi, na miili yao kama mavi.


Hapo hasira yangu itawawakia siku hiyo, nami nitawaacha na kuficha uso wangu mbali nao, wataangamizwa. Maovu mengi na taabu zitawapata hata watambue kwamba maovu hayo yamewapata kwa sababu Mungu wao hayuko kati yao.


Hakika nitawaficha uso wangu kwa sababu wamefanya mambo maovu na kugeukia miungu mingine.


Wanajikaza kutuzuiza tusitangaze Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine kusudi wasiokoke. Hivi wanafikilia kwenye hatua ya mwisho ya zambi walizotenda siku zote. Lakini kwa mwisho kasirani ya Mungu imewaangukia.


Kisha nikaona kiti kikubwa cheupe cha kifalme pamoja na yule aliyeikaa juu yake. Dunia na mbingu vikatoweka mbele yake navyo havikuonekana tena.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ