Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi. Mupumbafu anajisemesha hivi katika moyo: “Hakuna Mungu.” Wote wamepotoka kabisa, matendo yao ni ya kuchukiza; hakuna hata mumoja anayetenda mazuri!
Ninyi munajidai mumefanya agano na kifo mumefanya mapatano na kuzimu! Ninyi munasema kwamba hasara itakapokuja haitawapata, kwa sababu mumefanya uongo kuwa tegemeo lenu, na udanganyifu kuwa kikingio chenu!
Maana, inchi imejaa wazinzi. Kwa sababu ya laana, inchi inaomboleza, na mashamba ya kulishia nyama yamekauka. Mienendo ya watu ni miovu, wanapoteza nguvu kwa ajili ya mambo yasiokuwa ya haki.
Lakini kati ya manabii wa Yerusalema, nimeona mambo ya kutisha zaidi: wao wanafanya uzinzi na kusema uongo; wanawaunga mukono wanaotenda maovu hata kusikuwe mutu anayeachana na uovu. Kwangu wote wamekuwa kama watu wa Sodoma; wakaaji wake wamekuwa kama watu wa Gomora.
Mutu anaweza kujificha pahali pa siri hata nisiweze kumwona? –Ni ujumbe wa Yawe!– Hamujui kwamba niko kila pahali, katika mbingu na katika dunia? –Ni ujumbe wa Yawe!–
Yehudi alipokuwa amekwisha kusoma vipindi vitatu au vine hivi vya kitabu kile, mufalme alivikatakata kwa kisu na kuvitupa katika moto wa makaa. Aliendelea kufanya hivyo mpaka kitabu chote kikateketezwa.
manabii wanatabiri mambo ya uongo, nao makuhani wanatafuta faida yao wenyewe; nao watu wangu wanaona jambo hilo kuwa sawa. Lakini mwisho wake utakapofika mutafanya nini?
Kwa sababu mumewavunja watu wa haki moyo kwa kusema uongo, ijapokuwa mimi sikuwavunja moyo, mukawaimarisha waovu wasiache mienendo yao mibaya na kuokoa maisha yao,
Wakati huo nitauchunguza Yerusalema kwa taa, nitawaazibu wanaoishi wakitulia kama machicha ya divai, wote ambao wanasema kati yao: Yawe hatafanya kitu: chema au kibaya.