Ukubwa ni wako, ee Yawe, una nguvu, utukufu, ushindi na mamlaka. Vyote vinavyokuwa mbinguni na katika dunia ni vyako. Ee Yawe, ufalme ni wako, nawe umetukuzwa, uko mukubwa juu ya vitu vyote.
Nitatumia sheria kama kipimo changu, nitatumia haki kama timazi. Mvua ya mawe itaufagilia mbali uongo munaoutegemea, na mafuriko yataharibu kikingio chenu.
Watakapowaona watoto wao, watoto niliowajalia mimi mwenyewe, watalitukuza jina langu mimi Mutakatifu wa Yakobo, watakuwa na heshima kwangu mimi Mungu wa Israeli.
Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.
Sema hivi: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi nitapingana nawe Sidona, na kuonyesha utukufu wangu kati yako. Nitakapotimiza hukumu zangu juu yako na kukuonyesha utakatifu wangu, halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe.
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitawakusanya na kuwaleta Waisraeli kutoka katika mataifa yote ambamo walisambazwa. Hivyo nitawafanya watu wa mataifa waone kwamba mimi ni mutakatifu. Waisraeli wataishi katika inchi yao ambayo mimi nilimupa mutumishi wangu Yakobo.
Nitalitakasa jina langu kubwa mulilokufuru kati ya mataifa. Na kwa hiyo mataifa yatatambua kwamba mimi ni Yawe. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Nitawatumia ninyi kuonyesha utakatifu wangu mbele yao.
Utawashambulia Waisraeli, kama vile wingu linalotanda juu ya inchi. Wakati huo nitakutuma uishambulie inchi yangu, kusudi mataifa yajue kwamba nimekutumia wewe Gogi kusudi nionyeshe utakatifu wangu mbele yao.
Kwa hiyo, Musa akamwambia Haruni: Kwa tukio hili Yawe amekuonyesha maana ya kile alichosema: Nitajionyesha kuwa mutakatifu kati ya wale wanaokuwa karibu nami, nitatukuzwa mbele ya watu wote! Haruni akanyamaza kimya.
Lakini mumutukuze Bwana wenu Kristo ndani ya mioyo yenu. Mukuwe tayari wakati wowote kumujibu kila mutu anayewauliza juu ya tumaini munalokuwa nalo. Lakini mufanye vile kwa upole na heshima,
“Umwandikie malaika wa kanisa la Filadelfia hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayekuwa mutakatifu na mwenye ukweli, anayekuwa na ufunguo wa mufalme Daudi, anayefungua mulango wala hakuna anayeweza kuufunga, anayefunga wala hakuna anayeweza kuufungua.
Na kila kimoja cha viumbe vya ajabu kilikuwa na mabawa sita yenye kujaa macho ndani na inje. Navyo viliimba muchana na usiku bila kuchoka, vikisema: “Mutakatifu, mutakatifu, mutakatifu ni Bwana wetu, Mungu Mwenye Uwezo, aliyekuwa, anayekuwa na anayekuja.”