Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 5:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Lakini Yawe wa majeshi anatukuzwa wakati sheria yake inafuatwa. Utakatifu wa Mungu Mutakatifu unaonyeshwa wakati haki inatendwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 5:16
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ukubwa ni wako, ee Yawe, una nguvu, utukufu, ushindi na mamlaka. Vyote vinavyokuwa mbinguni na katika dunia ni vyako. Ee Yawe, ufalme ni wako, nawe umetukuzwa, uko mukubwa juu ya vitu vyote.


Kwa maana wewe utapiga mishale mbele yao, utawakimbiza mbio.


Anakomesha vita popote katika dunia. Anavunjavunja pinde na mikuki, nayo magari ya vita anayateketeza.


Mataifa yameanguka katika shimo walilochimba, miguu yao imenaswa kwenye wavu waliotega.


Siku hiyo mutasema: Mumushukuru Yawe, muombe kwa jina lake. Mujulishe kwa mataifa matendo yake, mutangaze kuwa jina lake limetukuzwa.


Macho yenye kiburi ya wanadamu yatanyenyekezwa, watu wenye majivuno watashushwa chini, na Yawe peke yake atatukuzwa siku hiyo.


Kiburi cha wanadamu kitashushwa, majivuno ya watu yatanyenyekezwa, na Yawe peke yake atatukuzwa siku hiyo.


Kwa hiyo, kila mutu atapata haya na kufezeheshwa. Usiwasamehe hata kidogo, ee Mungu!


Nitatumia sheria kama kipimo changu, nitatumia haki kama timazi. Mvua ya mawe itaufagilia mbali uongo munaoutegemea, na mafuriko yataharibu kikingio chenu.


Watakapowaona watoto wao, watoto niliowajalia mimi mwenyewe, watalitukuza jina langu mimi Mutakatifu wa Yakobo, watakuwa na heshima kwangu mimi Mungu wa Israeli.


Hata hivyo, Yawe anangoja kuwasamehe, atasimama na kuwaonea huruma. Yawe ni Mungu wa haki. Heri wote wale wanaomutumainia.


Yawe anasema hivi: Sasa mimi nitasimama; sasa nitajiweka tayari; sasa mimi nitatukuzwa.


Yawe ametukuzwa, yeye anaishi juu mbinguni. Ameujaza Sayuni usawa na haki.


Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.


Walilalamikiana mumoja kwa mwengine hivi: Mutakatifu, mutakatifu, mutakatifu ni Yawe wa majeshi! Dunia yote imejaa utukufu wake.


Mimi Yawe ninapenda watu wafuate sheria yangu; ninachukia unyanganyi na uovu. Nitawatunza watu wangu kwa uaminifu, nitafanya nao agano la milele.


Munitambue mimi peke yangu, Yawe wa majeshi, kuwa mutakatifu. Muniogope na kuniabudu mimi peke yangu.


Kisha kuwatoa toka katika inchi ambako mumesambazwa na kuwakusanya pamoja, nitazipokea sadaka zenu zenye harufu nzuri. Nami nitaonyesha utakatifu wangu kati yenu mbele ya mataifa mengine.


Sema hivi: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi nitapingana nawe Sidona, na kuonyesha utukufu wangu kati yako. Nitakapotimiza hukumu zangu juu yako na kukuonyesha utakatifu wangu, halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitawakusanya na kuwaleta Waisraeli kutoka katika mataifa yote ambamo walisambazwa. Hivyo nitawafanya watu wa mataifa waone kwamba mimi ni mutakatifu. Waisraeli wataishi katika inchi yao ambayo mimi nilimupa mutumishi wangu Yakobo.


Nitalitakasa jina langu kubwa mulilokufuru kati ya mataifa. Na kwa hiyo mataifa yatatambua kwamba mimi ni Yawe. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Nitawatumia ninyi kuonyesha utakatifu wangu mbele yao.


Utawashambulia Waisraeli, kama vile wingu linalotanda juu ya inchi. Wakati huo nitakutuma uishambulie inchi yangu, kusudi mataifa yajue kwamba nimekutumia wewe Gogi kusudi nionyeshe utakatifu wangu mbele yao.


Ndivyo nitakavyofanya kusudi yote yaone ukubwa wangu na utakatifu wangu. Halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Kwa hiyo, Musa akamwambia Haruni: Kwa tukio hili Yawe amekuonyesha maana ya kile alichosema: Nitajionyesha kuwa mutakatifu kati ya wale wanaokuwa karibu nami, nitatukuzwa mbele ya watu wote! Haruni akanyamaza kimya.


Hayo ni maji ya Meriba, ni kusema ya “Magombano”, pahali ambapo Waisraeli walimugombanisha Yawe, naye akajionyesha kwa utakatifu kati yao.


Lakini wewe ni mugumu na mwenye moyo usiotaka kugeuka. Kwa hiyo unajiwekea azabu kubwa siku Mungu atakapoonyesha kasirani yake na hukumu yake ya haki.


Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Muwe watakatifu, kwa maana mimi ni mutakatifu.”


Na hayo ndiyo mapenzi ya Mungu, anayetaka munyamazishe usemi wa ujinga wa wapumbafu kwa njia ya kutenda mema.


Lakini mumutukuze Bwana wenu Kristo ndani ya mioyo yenu. Mukuwe tayari wakati wowote kumujibu kila mutu anayewauliza juu ya tumaini munalokuwa nalo. Lakini mufanye vile kwa upole na heshima,


“Umwandikie malaika wa kanisa la Filadelfia hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayekuwa mutakatifu na mwenye ukweli, anayekuwa na ufunguo wa mufalme Daudi, anayefungua mulango wala hakuna anayeweza kuufunga, anayefunga wala hakuna anayeweza kuufungua.


Na kila kimoja cha viumbe vya ajabu kilikuwa na mabawa sita yenye kujaa macho ndani na inje. Navyo viliimba muchana na usiku bila kuchoka, vikisema: “Mutakatifu, mutakatifu, mutakatifu ni Bwana wetu, Mungu Mwenye Uwezo, aliyekuwa, anayekuwa na anayekuja.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ