Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 5:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Kwa hiyo, watu wangu watapelekwa katika uhamisho kwa sababu ya ukosefu wao wa akili. Wakubwa wao watakufa na njaa, watu wengi watakufa na kiu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 5:13
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea, mufalme wa Asuria aliuteka muji wa Samaria na kuwapeleka watu wa Israeli katika uhamisho mpaka Asuria. Wamoja kati yao akawaweka katika muji wa Hala, wengine karibu na muto Habori, muto Gozani na wengine katika miji ya Wamedi.


Maneno ya mwenye haki yanawafalia watu wengi, lakini wapumbafu wanakufa kwa kukosa akili.


Ngombe anamufahamu mwenye naye, punda anajua kibanda cha bwana wake; lakini Waisraeli hawajui, watu wangu, hawaelewi!


Inchi yenu imeharibiwa kabisa; miji yenu imeteketezwa kwa moto. Wageni wamebeba mazao ya inchi yenu mbele ya macho yenu, imeharibiwa kama vile Sodoma.


Ni Yawe wa majeshi! Yeye ndiye aliyeyapanga haya yote. Alifanya hivyo akiharibu kiburi chao na kuwapatisha haya waheshimiwa wake.


Matawi ya miti yamekauka na kuvunjika; wanawake wanayaokota na kuyawasha moto. Watu hawa hawajaelewa kitu, kwa hiyo Mungu, Muumba wao, hatawahurumia, yeye aliyewafanya, hatawatendea mema.


Sasa, Bwana wetu Yawe wa majeshi ataondoa kutoka Yerusalema na inchi ya Yuda kila tegemeo: tegemeo lote la chakula na la kinywaji.


majemadari na wakubwa, washauri, wachawi wafundi na waganga wenye maarifa.


Hakuna anayeweza kuwaza au kuwa na akili na kufikiri na kusema: Kipande cha muti huo nilikikonga moto; tena nikachoma mikate juu ya makaa yake, nikachoma nyama, nikakula. Basi, sehemu iliyobaki namna gani nitatengeneza nayo sanamu ambayo ni chukizo na kuabudu hicho kipande cha muti?


Kwa hiyo utajiuliza mwenyewe: Nani aliyenizalia watoto hawa wote? Nilikufiwa na watoto bila kupata wengine. Nilipelekwa katika uhamisho na kutupwa mbali; nani basi aliyewalea watoto hawa? Mimi niliachwa peke yangu, sasa, hawa wametoka wapi?


Basi, mimi Yawe ninasema: Watumishi wangu watakula, lakini ninyi mutasikia njaa; watumishi wangu watakunywa, lakini ninyi mutasikia kiu; watumishi wangu watafurahi, lakini ninyi mutafezeheka.


Nikienda inje katika mbuga, ninaiona maiti ya waliouawa kwa vita; nikiingia ndani katika muji, ninaona tu maiti ya waliokufa kwa njaa! Manabii na makuhani wanashugulikia mambo yao katika inchi, lakini hawajui wanalofanya.


Wakubwa wake wanawatuma watumishi wao maji; watumishi wanakwenda kwenye visima, lakini hawapati maji; wanarudi na vyombo vitupu. Kwa ajili ya haya na mahangaiko wanaangalia chini.


Hata korongo anajua wakati wa kuhama; njiwa, mbaruwayi na koikoi, wanajua nyakati zao za kurudi. Lakini hawa watu wangu hawajui maagizo ya Yawe.


Afazali waliouawa kwa upanga kuliko waliokufa kwa njaa, ambao walikufa polepole kwa kukosa mazao ya shamba.


Wakati umetimia, ile siku imekaribia. Mununuzi asifurahi wala muchuuzi asiomboleze; kwa sababu kasirani yangu itawaangukia watu wote.


Watu wangu wameangamia kwa kutonijua, maana wewe kuhani umekataa mafundisho. Nimekukataa kuwa kuhani wangu. Kwa maana umeisahau sheria ya Mungu wako, nami vilevile nitawasahau watoto wako.


Siku hiyo, wabinti wazuri na vijana wanaume watazimia kwa kiu.


Watakuharibu kabisa pamoja na wakaaji wako. Hawatakuachia hata jengo moja lisilobomolewa kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuja kukuokoa.”


Hivi kufuatana na vile walivyokataa kumutambua Mungu, Mungu akawaacha wafuate akili yao ya upotevu, kusudi wafanye mambo wasiyopaswa kufanya.


Watu hawa wanasahau kwa makusudi kwamba tangia zamani Mungu alisema tu, na mbingu na dunia vikakuwa. Dunia iliumbwa toka katika maji na kwa njia ya maji.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ