Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 49:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Watu wa Yerusalema wanalalamika: Shujaa, anaweza kunyanganywa vitu alivyoteka? Au wafungwa wa mutu mutesaji wanaweza kuokolewa?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 49:24
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata nyuma ya yote yaliyotupata kwa sababu ya maovu yetu na makosa yetu mengi, tunajua kwamba azabu uliyotupa, ee Mungu wetu, ni ndogo ikilinganishwa na makosa yetu, na umewaacha wazima wamoja kati yetu.


Haukutuacha tuishi katika utumwa ingawa tulikuwa watumwa. Uliwafanya wafalme wa Persia wakuwe wema kwetu na kuturuhusu tuishi na kuijenga nyumba yako iliyokuwa imebomoka, na ukatufanya tukae salama hapa Yuda na Yerusalema.


Hata hivyo, una haki kwa kutuazibu hivyo; maana wewe umekuwa mwaminifu wakati sisi tumekuwa watenda maovu.


Kwa sababu ya zambi zetu, utajiri wa inchi hii unawaendea wafalme uliowaleta kwa kututawala. Wanatutawala jinsi wanavyopenda hata na nyama wetu wa ufugo wanawatendea jinsi wanavyopenda, tuko katika taabu kubwa sana.


Lakini hawa ni watu walioibwa mali yao na kunyanganywa! Wote wamenaswa katika mashimo, wamefungwa katika kifungo. Wamenyanganywa bila mutu wa kuwaokoa, wamekamatwa mateka na hakuna anayesema: Muwarudishe!


Waaskari wao wananguruma kama simba; wananguruma kama simba wakali ambao wamekamata nyama wao na kuwapeleka mbali ambapo hakuna anayeweza kuwanyanganya.


Kwa hiyo nitamugawanyia sehemu pamoja na wakubwa, atagawanya vitu vilivyotekwa pamoja na wenye nguvu. Alijitoa yeye mwenyewe hata kufa; aliwekwa kundi moja na watu wakosaji. Alizibeba zambi za watu wengi, akawaombea musamaha hao wakosaji.


Kwa hiyo Yawe akaniambia: Wewe mwanadamu! Mifupa hiyo ni mufano wa watu wote wa inchi ya Israeli. Wao, wanasema: Mifupa yetu imekauka, matumaini yetu yamepotea nasi tumekwisha kabisa.


Yawe akaniuliza hivi: Wewe mwanadamu! Mifupa hii inaweza kuishi tena? Nami nikamujibu: Ee Bwana wetu Yawe, wewe unajua!


Simba dume amewararulia watoto wake nyama ya kutosha, akiwakamatia simba dike nyama zao; ameyajaza mapango yake na nyama, na makao yake vipande vya nyama.


“Hakuna mutu anayeweza kuingia ndani ya nyumba ya mwenye nguvu na kunyanganya vitu vyake, isipokuwa kwanza anamufunga. Na kisha anaweza kunyanganya vitu vyake vyote.


“Mutu hawezi kuingia ndani ya nyumba ya mwenye nguvu na kunyanganya vitu vyake, isipokuwa kwanza anamufunga. Kisha anaweza kunyanganya vitu vyake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ