Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 49:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Kwa hiyo utajiuliza mwenyewe: Nani aliyenizalia watoto hawa wote? Nilikufiwa na watoto bila kupata wengine. Nilipelekwa katika uhamisho na kutupwa mbali; nani basi aliyewalea watoto hawa? Mimi niliachwa peke yangu, sasa, hawa wametoka wapi?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 49:21
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sayuni umeachwa kama kibanda katika shamba la mizabibu, kama kibanda cha mulinzi katika shamba la maboga, kama muji uliozungukwa kwa vita.


Muji ule wenye kuta sasa umekuwa mutupu, umeachwa na kuhamwa kama jangwa, humo ngombe wanakula na kupumzika.


Watakapowaona watoto wao, watoto niliowajalia mimi mwenyewe, watalitukuza jina langu mimi Mutakatifu wa Yakobo, watakuwa na heshima kwangu mimi Mungu wa Israeli.


Halafu watu watalia na kuomboleza kwenye milango ya muji; nao wataikaa ndani ya mavumbi katika ukiwa.


Kwa hiyo, watu wangu watapelekwa katika uhamisho kwa sababu ya ukosefu wao wa akili. Wakubwa wao watakufa na njaa, watu wengi watakufa na kiu.


Ujikungute mavumbi, usimame, ewe Yerusalema uliyekuwa mufungwa! Ujifungue minyororo yako katika shingo, ewe binti Sayuni uliyekamatwa mateka.


Wewe ulikuwa umeachwa na kuchukiwa, hakuna aliyependa hata kupita ndani yako. Lakini sasa nitakufanya ukuwe na utukufu milele, utakuwa muji wa furaha kwa kizazi na kizazi.


Nani hao wanaopita mbio kama mawingu, kama njiwa wanaoruka kwenda katika chicha zao?


Hautaitwa tena: Aliyeachwa, wala inchi yako haitaitwa: “Ukiwa”. Lakini utaitwa: “Ninamufurahia”, na inchi yako itaitwa: “Aliyeolewa”. Maana Yawe amependezwa nawe, naye atakuwa kama mume wa inchi yako.


Nyumba yetu takatifu na nzuri, ambamo babu zetu walikusifu, imeteketezwa kwa moto. Pahali petu pote pazuri pamekuwa mabomoko.


Wamoja watauawa kwa vita na watapelekwa kuwa wafungwa katika inchi za mataifa yote. Vilevile mataifa mengine yatautawala Yerusalema mpaka nyakati zao za kuutawala zitakapokwisha.”


Ninyi watu wa mataifa mengine ni kama tawi la muzeituni wa pori lililokatwa na kisha likapandikizwa ndani ya muzeituni uliopandwa, umbalimbali na kawaida. Wayuda ni kama muzeituni huu uliopandwa; na si neno gumu basi kwa Mungu kupandikiza tena matawi yaliyokatwa katika muti wao wenyewe.


Kama ninyi ni watu wa Kristo, basi, ninyi ni wazao wa Abrahamu, ninyi mutakuwa warizi sawa vile Mungu alivyoahidi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ