Yawe anasema hivi: Wakati uliofaa nilijibu maombi yako; wakati wa wokovu nilikusaidia. Nimekuweka na kukufanya ukuwe kiungo cha agano langu na mataifa yote: utatengeneza inchi na kurudisha tena inchi hiyo iliyoharibika.
Nitalifanya ukiwa kabisa, mizabibu yake haitasafishwa matawi wala kupaliliwa. Litaota michongoma na miiba. Tena nitayaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.
Mimi Yawe nitaufariji Sayuni, nitatengeneza pahali pake pote palipoharibika. Nitazifanya mbuga zake kama shamba la Edeni, jangwa yake kama bustani ya Yawe. Ndani yake kutapatikana furaha na shangwe, na nyimbo za shukrani zitasikilika humo.
Lakini wote wanaokuangamiza, wataangamizwa vilevile, na waadui zako wote watapelekwa katika uhamisho; nao wanaokukamata mateka watakamatwa mateka, nao wanaokuwinda, nitawawinda.
Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Babeli ni kama uwanja wa kupepetea ngano wakati unapotayarishwa. Lakini bado kidogo tu, wakati wa mavuno utaufikia.
Kwa hiyo, wewe Ezekieli, toa unabii useme kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Watu wamewafanya ninyi milima ya Waisraeli kuwa tupu na kuwashambulia kutoka kila upande hata mumekuwa mali ya mataifa mengine, mukakuwa kitu cha kusimangwa na kuchekelewa kati ya watu!
Nitawarudisha kutoka inchi ya Misri, nitawakusanya kutoka Asuria; nitawaleta katika inchi ya Gileadi na Lebanoni, nao watajaa kila nafasi katika inchi.
Nami nikauliza: Watu hawa wanakuja kufanya nini? Yeye akanijibu: Watu hawa wamekuja kuyatisha na kuyaangamiza yale mataifa yenye nguvu ambayo yaliishambulia inchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.
Basi, huyo malaika aliyezungumuza nami akamwambia yule mwenzake: Kimbia umwambie yule kijana kwamba si lazima Yerusalema ukuwe na kuta, kama sivyo hapatakuwa nafasi ya kuwatoshelea wakaaji wake wengi na nyama watakaokuwa ndani yake.