Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 49:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Inua macho uangalie pande zote; watu wako wote wanakusanyika na kukufikia. Kama vile ninavyoishi, watu wako watakuwa kwako kama mapambo, utawafurahia kama vile bibi arusi anavyofanya na taji lake. –Ni ujumbe wa Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 49:18
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nyuma ya Loti kujitenga na Abramu, Yawe akamwambia Abramu: “Inua macho yako toka pale unapokuwa, utazame pande zote: kaskazini, kusini, mashariki na magaribi.


akamwambia: “Yawe anasema hivi: Nimeapa kwa nafsi yangu mwenyewe kwamba kwa sababu umefanya hivi, wala haukuninyima mwana wako wa pekee,


Taji la sifa la wazee ni wajukuu wao. Heshima ya wana ni baba yao.


Mimi nimeapa kwa nafsi yangu, ninachosema ni ukweli, neno langu halitarudi nyuma: kila mwanadamu atanipigia magoti, kila mutu atafanya kiapo.


Watu wangu watarudia kutoka mbali, wengine kutoka kaskazini na magaribi, wengine kutoka upande wa kusini.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitasimika bendera kwa kuita mataifa; nitayaonyesha kitambulisho. Nayo yatawarudishia wana wenu wakiwabeba kwenye kifua, vilevile na wabinti zenu kwenye mabega.


Amuka! Amuka! Ujipatie zile nguvu zako, ewe Sayuni! Uvae nguo yako nzuri, ewe Yerusalema, muji mutakatifu. Maana hawataingia tena kwako watu wasiotahiriwa na wachafu.


Nilikuacha kwa muda mufupi tu. Kwa huruma nyingi, nitakurudisha.


Nitafanya kama nilivyofanya wakati wa Noa. Wakati ule niliapa kwamba sitaifunika tena dunia kwa mafuriko ya maji. Basi sasa ninaapa kwamba sitakukasirikia tena wala sitakukaripia tena.


Nitafurahi sana kwa sababu ya Yawe, nafsi yangu itashangilia kwa sababu ya Mungu wangu. Maana amenivalisha nguo ya wokovu, amenifunika kanzu ya haki, kama bwana arusi anavyojipamba kwa shada la maua, kama bibi arusi anavyojipamba kwa ushanga wake.


Watawarudisha wandugu zenu wote kutoka katika mataifa yote kama matoleo yangu mimi Yawe. Watawaleta juu ya farasi, juu ya nyumbu, juu ya ngamia na ndani ya magari na juu ya vipoyi mpaka Yerusalema, kwenye mulima wangu mutakatifu. Watawaleta kama Waisraeli wanavyoleta sadaka ya unga katika chombo safi mpaka ndani ya nyumba yangu mimi Yawe.


Kijana binti anaweza kusahau mapambo yake, au bibi arusi nguo yake? Lakini watu wangu wamenisahau kwa muda wa siku zisizohesabika.


Nitawarudisha kutoka inchi ya kaskazini, nitawakusanya kutoka miisho ya dunia. Wote watakuwa pale; hata vipofu na vilema, wanawake wenye mimba na wanaosikia maumivu ya kuzaa; kundi kubwa sana la watu litarudi hapa.


Mimi nitawasha moto katika mahekalu ya miungu ya Misri; naye Nebukadneza ataiteketeza miungu hiyo kwa moto au kuikamata mateka mpaka Babeli. Ataisafisha inchi ya Misri kama muchungaji anavyoondoa vidudu katika nguo yake na kuondoka Misri akiwa mushindi.


Basi, uwaambie: Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– mimi sikifurahii kifo cha mutu mwovu, lakini ninapenda mutu mwovu aachane na mwenendo wake mubaya, apate kuishi. Mugeuke, muachane na mwenendo wenu mubaya, enyi Waisraeli! Kwa nini munataka kufa?


Lakini kwa kweli, kama vile ninavyoishi na kama vile dunia itakavyojaa utukufu wa Yawe,


Si ninyi munazoea kusema: ‘Kunabaki miezi mine kuwe mavuno’? Lakini mimi ninawaambia, muinue macho, muangalie mashamba; mimea imekomaa, nayo ni tayari kwa kuvunwa.


Nikaona muji mutakatifu, ndio Yerusalema mupya, uliokuwa ukishuka toka mbinguni kwa Mungu, nao ukitengenezwa vizuri kama vile bibi arusi aliyepambwa kwa ajili ya kwenda kukutana na mume wake.


Lakini mbali ya muji ule kuna watu wenye kuchukiza, wachawi, wazinzi, wauaji, wanaobudu sanamu na wasema uongo na wote wanaoupenda.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ