Na mambo haya yatakuwa ukumbusho, kama vile kitambulisho katika mikono yenu au katika paji la nyuso zenu; kusudi kiwakumbushe siku zote sheria ya Yawe. Maana, Yawe amewatoa katika inchi ya Misri kwa mukono wenye nguvu.
Unipige kama muhuri ndani ya moyo wako, kama muhuri katika mikono yako. Maana mapendo yana nguvu kama kifo, nao wivu ni mukali kama kaburi. Kuwaka kwake ni kama kuwaka kwa moto, unawaka kama ulimi wa moto.
Mateso makali hayatasikilika tena katika inchi yako; wala uharibifu na maangamizi ndani ya mipaka yako. Utaweza kuziita kuta zako: “Wokovu”, na milango yako: “Sifa”.
Zambi ya watu wa Yuda, haiwezi kufutikana, imeandikwa kwa kalamu ya chuma; kwa chongo ya almasi. Imechorwa ndani ya mioyo yao na kwenye pembe za mazabahu yao.
Yawe anasema hivi: Kama vile ninavyoishi, hata kama wewe Konia mwana wa Yoyakimu, mufalme wa Yuda, ungekuwa wa lazima kwangu kama vile pete yangu ya muhuri ninayovaa kwa mukono wangu wa kuume, ningekuvua.
Siku hiyo, nitakutwaa wewe Zerubabeli mwana wa Saltieli, mutumishi wangu. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi! Nitakusimika utawale kwa jina langu. –Ni ujumbe wa Yawe! Wewe ndiwe niliyekuchagua. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi!