Muimbe kwa furaha, enyi mbingu! Ushangilie ewe dunia, Enyi milima, mulalamike kwa furaha, maana Yawe amewafariji watu wake, anawaonea huruma watu wake wanaoteseka.
Lakini Yawe anasema: Munafikiri kwamba mama anaweza kumusahau mutoto anayemunyonyesha, wala kumuchukia mutoto wa tumbo lake? Hata kama mama anaweza kumusahau mutoto wake, mimi sitakusahau hata kidogo.
Ewe mwanadamu! Uwaambie Waisraeli jambo hili: Ninyi munasema: Tumezidiwa na makosa na zambi zetu. Tunaregea kwa sababu yake! Tutaweza namna gani kuishi?