Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 49:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Muimbe kwa furaha, enyi mbingu! Ushangilie ewe dunia, Enyi milima, mulalamike kwa furaha, maana Yawe amewafariji watu wake, anawaonea huruma watu wake wanaoteseka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 49:13
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufurahi enyi mbingu na dunia! Muambie mataifa: “Yawe anatawala!”


Mumusifu, enyi milima na vilima, miti ya matunda na ya mierezi!


Mbuga za majani zimejaa mifugo, milima nayo imejaa furaha.


Yawe anawasikiliza wakosefu; hatawasahau hata kidogo watu wake wafungwa.


Utaniongezea heshima yangu, na kunifariji tena.


Wewe uliumba kaskazini na kusini; milima Tabori na Hermoni inakushangilia.


Siku hiyo mutasema: Ninakushukuru, ee Yawe, maana ingawa ulinikasirikia, hasira yako imetoweka, nawe umenifariji.


Yawe atawahurumia tena watu wa Yakobo, atawachagua tena Waisraeli. Atawarudisha katika inchi yao wenyewe, na wageni watakuja na kukaa pamoja na watu wa Yakobo.


Muimbe kwa furaha enyi mbingu, kwa sababu ya yale Yawe aliyotenda. Mupige kelele enyi vilindi vya dunia! Mupige vigelegele enyi milima! Enyi mapori na miti yote inayokuwa ndani yake, mushangilie. Maana Yawe amewakomboa wazao wa Yakobo, naye atatukuzwa katika inchi ya Israeli.


Sasa, muondoke Babeli! Mukimbie kutoka kwa Wakaldea! Mutangaze jambo hili kwa sauti za shangwe. Mueneze habari zake kila pahali katika dunia. Museme: Yawe amekomboa taifa la mutumishi wake Yakobo.


Wewe Sayuni unasema: Yawe ameniacha. Hakika Bwana wangu amenisahau.


Yawe anasema hivi: Mimi, kweli mimi, ndiye ninayekufariji. Kwa nini wewe unamwogopa mutu ambaye ni wa kufa, mwanadamu ambaye anatoweka kama majani?


Mimi Yawe nitaufariji Sayuni, nitatengeneza pahali pake pote palipoharibika. Nitazifanya mbuga zake kama shamba la Edeni, jangwa yake kama bustani ya Yawe. Ndani yake kutapatikana furaha na shangwe, na nyimbo za shukrani zitasikilika humo.


Mupige kelele za shangwe, enyi mabomoko ya Yerusalema! Yawe amewafariji watu wake, ameukomboa Yerusalema.


Nilikuacha kwa muda mufupi tu. Kwa huruma nyingi, nitakurudisha.


Kwa hasira nyingi nilikuficha uso wangu kwa muda kidogo, lakini kwa wema wa milele nitakuonea huruma. Ni Yawe Mukombozi wako anayesema hivyo.


Mutatoka Babeli kwa furaha; mutaongozwa muende kwa amani. Milima na vilima mbele yenu vitapiga kelele na kuimba, na miti yote katika mashamba itawapigia mikono.


Halafu wabinti zao watafurahi na kucheza, vijana na wazee watashangilia kwa furaha. Nitageuza maombolezo yao kuwa furaha, nitawafariji na kuwapa furaha pahali pa huzuni.


Kisha mbingu, dunia na vyote vinavyokuwa ndani yao vitaimba kwa furaha juu ya kuanguka kwa Babeli, wakati waangamizaji watakapofika kutoka upande wa kaskazini kuushambulia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitakapokufanya wewe Edomu kuwa jangwa, dunia yote itafurahi


Vilevile ninawaambia, ndivyo wamalaika wa Mungu wanavyofurahi kwa ajili ya mwenye zambi mumoja anayegeuka toka zambi zake.”


Lakini Mungu anayefariji watu wanyenyekevu, ametufariji kwa njia ya kufika kwa Tito.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ