Wakati huo, kutakuwa barabara kubwa kutoka inchi ya Misri mpaka katika inchi ya Asuria. Waasuria watawatembelea Wamisri, na Wamisri watawatembelea Waasuria; nao wote watamwabudu Mungu pamoja.
Enyi wakaaji wa Yerusalema, mutoke, mutoke inje ya muji, muwatayarishie njia watu wenu wanaorudia! Mujenge! Mujenge barabara na kuondoa mawe yote! Muweke bendera kuwa kitambulisho kwa ajili ya watu.