Basi, mujumbe huyo alipokwenda alikutana na Yehu na kumwambia: “Mufalme anauliza: unakuja kwa amani?” Yehu akajibu: “Kwa nini unauliza juu ya amani? Wewe geuka ufuatane nami!” Mulinzi juu ya munara akasema: “Mujumbe amewafikia, lakini harudi.”
Halafu mujumbe wa pili akatumwa na kumwuliza Yehu: “Mufalme anauliza: unakuja kwa amani?” Yehu akajibu: “Kwa nini unauliza juu ya amani? Wewe geuka ufuatane nami!”
Munisikilize, enyi inchi za mbali, Mutege sikio, enyi watu wa mbali! Yawe aliniita mbele sijazaliwa, alitaja jina langu nikiwa katika tumbo la mama yangu.
Kisha watakwenda kuziona maiti za wale walioniasi. Wadudu watakaowakula hawatakufa, na moto utakaowachoma hautazimika hata kidogo. Watakuwa chukizo kwa watu wote.