Angalia mimi nitasimama mbele yako juu ya jiwe la mulima wa Horebu, nawe utapiga lile jiwe na maji yatabubujika kutoka mule kusudi watu wote wapate kunywa.” Basi, Musa akafanya hivyo mbele ya wazee wa Waisraeli.
Hawatasikia tena njaa wala kuwa na kiu. Upepo wenye kuunguza wala jua havitawachoma, mimi niliyewahurumia nitawaongoza na kuwapeleka kwenye chemichemi za maji.
Watarudi wakiwa wanatoa machozi, nami nitawaongoza nikiwafariji; nitawapitisha kando ya vijito vya maji, katika njia iliyonyooka ambamo hawatajikwaa; maana mimi nimekuwa baba wa Israeli, Efuraimu ni muzaliwa wangu wa kwanza.