Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 48:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Sasa, muondoke Babeli! Mukimbie kutoka kwa Wakaldea! Mutangaze jambo hili kwa sauti za shangwe. Mueneze habari zake kila pahali katika dunia. Museme: Yawe amekomboa taifa la mutumishi wake Yakobo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 48:20
39 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Tena, hakuna watu katika dunia ambao wanaweza kufananishwa na watu wako Waisraeli. Ulikwenda kuwakomboa kutoka Misri na miungu yake kusudi wakuwe watu wako. Ukawafanyia jina na kuwatendea mambo makubwa na ya ajabu.


Hawa ndio watu wa majimbo waliotoka katika utumwa ambao Nebukadneza mufalme wa Babeli aliwapeleka wafungwa Babeli, wakarudi katika Yerusalema katika inchi ya Yuda. Kila mutu alirudi katika muji wake.


Wimbo wa safari za kidini. Yawe alipoturudisha tena Sayuni, tulikuwa kama watu wanaoota ndoto!


Siku hiyo mutasema: Ninakushukuru, ee Yawe, maana ingawa ulinikasirikia, hasira yako imetoweka, nawe umenifariji.


Siku hiyo mutasema: Mumushukuru Yawe, muombe kwa jina lake. Mujulishe kwa mataifa matendo yake, mutangaze kuwa jina lake limetukuzwa.


Watu wanalalamika, wanaimba kwa shangwe. Kutoka upande wa magaribi, wanatangaza ukubwa wa Yawe,


Siku ile watu wataimba wimbo huu katika inchi ya Yuda: Sisi tuna muji imara: Mungu anatulinda kwa kuta na upango.


Mumwimbie Yawe wimbo mupya! Dunia yote iimbe sifa zake: bahari na vyote vinavyokuwa ndani yake, inchi za mbali na wakaaji wake;


Yawe aliyewaumba enyi watu wa Yakobo, yeye aliyewafanya enyi watu wa Israeli, anasema hivi: Musiogope, maana mimi nimewakomboa; nimewaita kwa jina lenu nanyi ni wangu.


Nimezimisha makosa yako nayo yametoweka kama mawingu, nimefuta zambi zako, nazo zimepotea kama kunguku. Urudi kwangu maana mimi nimekukomboa.


Wewe uliyasikia na sasa unayaona yote. Kwa nini hauwezi kuyakubali? Tangu sasa nitakujulisha mambo mapya; mambo yaliyofichwa ambayo haukuyajua.


Muimbe kwa furaha, enyi mbingu! Ushangilie ewe dunia, Enyi milima, mulalamike kwa furaha, maana Yawe amewafariji watu wake, anawaonea huruma watu wake wanaoteseka.


Yeye anasema: Haitoshi tu wewe kuwa mutumishi wangu, kusudi uyainue makabila ya Yakobo, na kurudisha watu wa Israeli waliobaki. Nitakufanya ukuwe mwangaza wa mataifa, kusudi watu wote wapate kuokolewa katika dunia.


Wafungwa watafunguliwa upesi, hawatakufa na kushuka katika shimo, wala hawatakosewa chakula.


Yawe ameonyesha nguvu yake tukufu, mbele ya mataifa yote. Atawaokoa watu wake, na ulimwengu wote utashuhudia.


Muondoke! Muondoke! Mutoke pale! Musiguse kitu chochote kichafu! Muondoke kule Babeli! Mujitakase, enyi munaobeba vyombo vya Yawe.


Mupige kelele za shangwe, enyi mabomoko ya Yerusalema! Yawe amewafariji watu wake, ameukomboa Yerusalema.


Yawe ametangaza katika dunia yote, muwaambie watu wa Sayuni hivi: Mukombozi wenu anakuja, yeye anakuja na mapato yake, anafika na mushahara wake.


Katika taabu zao zote, hakumutuma mujumbe mwingine kwa kuwasaidia, lakini yeye mwenyewe alikuja kuwaokoa; kwa upendo na huruma yake aliwakomboa. Aliwabeba na kuwakamata tangu zamani.


Enyi mataifa, musikilize neno langu mimi Yawe, mulitangaze katika visanga vya mbali, museme hivi: Aliyemusambaza Israeli, atamukusanya, atamutunza kama muchungaji anavyotunza kondoo wake.


Maana mimi Yawe nimemukomboa Yakobo, nimemwokoa kutoka kwa wenye nguvu kuliko yeye.


Weka kitambulisho katika njia zako, simika nguzo za kukuongoza, ukumbuke vema ile njia kubwa, barabara uliyopita ndani yake ukienda. Ewe Israeli rudi, rudi kwa nyumba katika miji yako.


Mutangaze kati ya mataifa, munyanyue bendera na kutangaza, musifiche jambo lolote. Museme: Babeli umetekwa, mungu Beli amepatishwa haya. Merodaki amefazaishwa; sanamu zake zimefezeheshwa, miungu yake imefazaishwa.


Sikiliza! Wakimbizi na wenye kutoroka kutoka inchi ya Babeli wanakuja kutangaza huko Sayuni jinsi Yawe, Mungu wetu, alivyolipiza kisasi kwa ajili ya hekalu lake.


Mukimbie kutoka Babeli! Mutoke inje ya ile inchi ya Wakaldea, mukuwe kama mabeberu mbele ya kundi.


Mutoke humo, enyi watu wangu! Kila mutu apate kuyaokoa maisha yake, kutoka hasira kali ya Yawe.


Kisha mbingu, dunia na vyote vinavyokuwa ndani yao vitaimba kwa furaha juu ya kuanguka kwa Babeli, wakati waangamizaji watakapofika kutoka upande wa kaskazini kuushambulia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Mukimbie kutoka Babeli, kila mutu apate kuyaokoa maisha yake! Musiangamizwe katika azabu yake, maana huu ndio wakati wa Mungu wa kulipiza kisasi, anaiazibu Babeli kama inavyostahili.


Nitawaita watu wangu na kuwakusanya pamoja; nimekusudia kuwakomboa, nao watakuwa wengi kama vile mbele.


Yawe anasema hivi: Mukimbie kutoka katika inchi ya kaskazini ambako mimi nilikuwa nimewatawanya kila upande.


Na hata kama mumetawanywa katika sehemu mbali kabisa katika dunia, Yawe, Mungu wenu, atawakusanya na kuwarudisha,


Enyi mbingu, nanyi watu wa Mungu pamoja na mitume na manabii wake, mufurahi kwa ajili ya mambo yaliyotokea muji ule, kwa maana Mungu amewapatia haki yenu kwa kuuhukumu!


Kisha nikasikia sauti ingine kutoka mbinguni ikisema: “Mutoke katika muji ule ninyi watu wangu, kusudi musishiriki zambi zake na kupatwa vilevile na mapigo yatakayoupata.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ