Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 48:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Yawe, Mutakatifu wa Israeli, Mukombozi wako, anasema hivi: Mimi ndiye Yawe, Mungu wako; ninayekufundisha kwa faida yako na kukuongoza katika njia unayotakiwa kwenda.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 48:17
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha nikainama na kumwabudu Yawe. Nikamutukuza Yawe, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye ameniongoza moja kwa moja kwa binti wa ukoo wa bwana wangu kwa ajili ya mwana wake.


tafazali, uwasikilize kutokea kule mbinguni, usamehe zambi za watumishi wako, watu wako Waisraeli, na uwafundishe kufuata njia nzuri. Kisha unyeshe mvua katika inchi yako hii ambayo uliwapa watu wako kwamba itakuwa mali yao.


Kumbuka ukubwa wa uwezo wa Mungu; nani anayeweza kufundisha kama yeye?


Kila mutu anayemwabudu Yawe, Yawe atamufundisha njia ya kufuata.


Mungu anasema: “Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayofuata. Nitakushauria kwa uangalifu mukubwa.


Ee Mungu, wewe umenifundisha tangu ujana wangu; tena na tena, ninatangaza matendo yako ya ajabu.


Wewe unaniongoza kwa mashauri yako; na kwa mwisho utanipokea kwenye utukufu.


watu wengi wataenda kule na kusema, Mukuje tupandie kwenye mulima wa Yawe, tuende kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo, apate kutufundisha njia zake, nasi tutafuata mapito yake. Maana sheria itakuja kutoka Sayuni; neno la Yawe kutoka Yerusalema.


Wao wananichekelea na kuuliza: Huyu nabii anataka kufundisha nani? Anazani atatuelezea sisi ujumbe wake? Sisi ni watoto wachanga walioachishwa kunyonya juzijuzi?


Ingawa Bwana atawakulisha chakula cha taabu na kuwakunywesha maji ya mateso, yeye ndiye Mwalimu wenu na hatajificha tena; nanyi mutamwona kwa macho yenu wenyewe.


Mukienda kwa upande wa kuume au kushoto, mutasikia sauti nyuma yenu ikisema: Njia ni hii; muifuate.


Enyi watu wa Yakobo zaifu kama mududu, enyi Waisraeli, musiogope! Nitawasaidia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Mukombozi wenu ni yule Mutakatifu wa Israeli.


Yawe, Mukombozi wenu, Mutakatifu wa Israeli, anasema hivi: Kwa ajili yenu nitatuma waaskari kwenda Babeli. Nitavunja vifungio vya milango ya muji wake, na kelele za wale Wakaldea zitageuka maombolezo.


Zamani Yawe alifanya barabara katika bahari na kuweka njia kati ya maji mengi. Alipiga kundi la waaskari lenye nguvu, kundi la magari na farasi wa vita, waaskari na mashujaa wa vita. Aliwaangusha chini hata hawawezi kusimama tena, Aliwakomesha na kuwazimisha kama utambi wa taa. Sasa Yawe anasema hivi:


Yawe, Mutakatifu wa Israeli, Mungu, Muumba wa Israeli anasema hivi: Munataka kuniuliza juu ya watoto wangu, au kuniamuru juu ya kazi zangu mwenyewe?


Sasa, muondoke Babeli! Mukimbie kutoka kwa Wakaldea! Mutangaze jambo hili kwa sauti za shangwe. Mueneze habari zake kila pahali katika dunia. Museme: Yawe amekomboa taifa la mutumishi wake Yakobo.


Nitawasukuma watesaji wako wakule miili yao wenyewe; watalewa damu yao wenyewe kama divai. Halafu wanadamu wote watatambua kwamba mimi ni Yawe, Mwokozi wako, Mukombozi wako, Mwenye Nguvu wa Yakobo.


Yawe, Mukombozi na Mutakatifu wa Israeli, anamwambia hivi yule anayezarauliwa sana, yule anayechukiwa na mataifa, na ambaye ni mutumishi wa watawala: Wafalme wataona nao watasimama; wakubwa watainama na kuabudu kwa heshima ya Yawe ambaye anatimiza ahadi zake, kwa heshima ya Mutakatifu wa Israeli ambaye amekuchagua wewe.


Watu wako watafundishwa nami Yawe, wana wako watapata ustawi mwingi.


Muumba wako atakuwa mume wako. Jina lake Yawe wa majeshi. Mukombozi wako ni Mutakatifu wa Israeli. Yeye anaitwa Mungu wa Ulimwengu Wote.


Kwa hasira nyingi nilikuficha uso wangu kwa muda kidogo, lakini kwa wema wa milele nitakuonea huruma. Ni Yawe Mukombozi wako anayesema hivyo.


Yawe anasema hivi: Musimame katika masanganjia, muangalie. Muulize juu ya matukio ya zamani. Mutafute pahali panapokuwa njia nzuri muifuate, nanyi mutaweza kupumzika. Lakini wao wakasema: Hatutafuata njia hiyo.


mataifa mengi yataufikia na kusema: Tuende juu kwenye mulima wa Yawe, tuende katika nyumba ya Mungu wa Yakobo, kusudi atufundishe njia zake, nasi tuzifuate. Maana sheria itatoka kule Sayuni; na neno la Yawe kule Yerusalema.


Imeandikwa hivi katika maandiko ya manabii: ‘Wote watafundishwa na Mungu.’ Kila mutu anayemusikia Baba na kufuata mafundisho yake, anakuja kwangu.


Hakika mumesikia habari zake, nanyi mukiwa waamini mumefundishwa kufuatana na ukweli unaokuwa ndani ya Kristo.


ndivyo mutakavyojua njia ya kupita maana hamujapita huku hata kidogo. Lakini musilikaribie sana Sanduku la Agano; mukuwe kwa umbali wa kilometre moja hivi.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ