Isaya 48:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 200217 Yawe, Mutakatifu wa Israeli, Mukombozi wako, anasema hivi: Mimi ndiye Yawe, Mungu wako; ninayekufundisha kwa faida yako na kukuongoza katika njia unayotakiwa kwenda. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Zamani Yawe alifanya barabara katika bahari na kuweka njia kati ya maji mengi. Alipiga kundi la waaskari lenye nguvu, kundi la magari na farasi wa vita, waaskari na mashujaa wa vita. Aliwaangusha chini hata hawawezi kusimama tena, Aliwakomesha na kuwazimisha kama utambi wa taa. Sasa Yawe anasema hivi:
Yawe, Mukombozi na Mutakatifu wa Israeli, anamwambia hivi yule anayezarauliwa sana, yule anayechukiwa na mataifa, na ambaye ni mutumishi wa watawala: Wafalme wataona nao watasimama; wakubwa watainama na kuabudu kwa heshima ya Yawe ambaye anatimiza ahadi zake, kwa heshima ya Mutakatifu wa Israeli ambaye amekuchagua wewe.