Kwa hiyo nilikutangazia mambo yale tangu zamani, mbele hayajatukia, mimi nilikujulisha, kusudi usiseme: Ni sanamu yangu iliyotenda mambo hayo, sanamu zangu za chuma ndizo ziliyaagiza.
Katika hali ya sasa ninapata faida gani kuwaona watu wangu wamepelekwa katika utumwa? –Ni ujumbe wa Yawe. Hao wanaowatawala wanajitapa. Nalo jina langu linaendelea kuzarauliwa kila siku. –Ni ujumbe wa Yawe.
Nao watu wanasema: Ingawa zambi zetu zinatoa ushuhuda juu yetu, utusaidie ee Yawe kwa ajili ya heshima ya jina lako. Maasi yetu ni mengi, tumetenda zambi mbele yako.
Lakini nilijizuiza kufanya hivyo kwa heshima ya jina langu kusudi lisizarauliwe kati ya watu wa mataifa ambao waliona jinsi nilivyowatoa Waisraeli katika inchi ya Misri.
Lakini nilizuiza mukono wangu kwa sababu ya heshima ya jina langu kusudi nisizarauliwe kati ya watu wa mataifa walioona nikiwatoa katika inchi ya Misri.
Na sasa, enyi Waisraeli, Bwana wenu Yawe anawaambia hivi: Muendelee kuziabudu sanamu zenu za miungu, kama hamunisikilizi; lakini mutalazimishwa kuacha kulikufuru jina langu takatifu kwa sadaka na sanamu zenu.
Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe, wakati nitakapowatendea ninyi sio kulingana na mwenendo wenu na matendo yenu mabaya, lakini kwa heshima ya jina langu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
Lakini nilijizuiza kufanya hivyo kwa heshima ya jina langu kusudi lisizarauliwe kati ya watu wa mataifa wanaoishi nao, hao walioona nikijijulisha kwa Waisraeli wakati wa kuwatoa katika inchi ya Misri.
Basi, uwaambie Waisraeli kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninachotaka kufanya si kwa faida yenu ninyi watu wa inchi ya Israeli, lakini ni kwa heshima ya jina langu takatifu mulilolikufuru kati ya mataifa mulikokwenda.
Kwa hiyo, ee Mungu, usikilize malalamiko yangu na maombi yangu mimi mutumishi wako. Kwa ajili ya heshima yako, ulionee tena hekalu lako lililoharibika huruma.