Isaya 47:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20028 Sasa, basi, sikiliza, ewe mupenda raha, wewe unayezani kuwa katika usalama, na kujisemesha: Mimi ndiye. Hakuna mwingine isipokuwa mimi. Sitakuwa mujane hata kidogo, wala sitakufiwa na watoto wangu. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Wewe utafukuzwa mbali na wanadamu. Utaishi pamoja na nyama wa pori, utakula majani kama ngombe; utalowana na umande wa mbinguni. Utakaa katika hali hiyo kwa miaka saba, na kwa mwisho utatambua kwamba Mungu Mukubwa ndiye anayetawala juu ya ufalme wa wanadamu naye anamupa ufalme ule mutu yeyote anayemutaka.
Pahali pake umejitukuza mwenyewe mbele ya Bwana wa mbinguni: umeleta vyombo vya nyumba ya Mungu ukavitumia kwa kunywea divai, wewe, wakubwa wako, wanawake wako na wahabara wako, na kuisifu miungu iliyotengenezwa na feza, zahabu, shaba, chuma, miti na mawe; miungu ambayo haioni, haisikii wala haijui jambo lolote. Lakini Mungu, ambaye uzima wako uko katika mukono wake, na njia zako ziko wazi mbele yake, haukumuheshimu!
Basi, watu hao watano wakaondoka, wakaenda Laisi. Waliwaona watu walioishi kule, na jinsi walivyokaa kwa usalama kama vile watu wa Sidona. Walikuwa watu watulivu wasiokuwa na wasiwasi na hawakupungukiwa mahitaji yoyote katika inchi. Walikuwa mbali na watu wa Sidona, na hawakukuwa na shuguli yoyote na watu wengine.