Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 47:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Sasa, basi, sikiliza, ewe mupenda raha, wewe unayezani kuwa katika usalama, na kujisemesha: Mimi ndiye. Hakuna mwingine isipokuwa mimi. Sitakuwa mujane hata kidogo, wala sitakufiwa na watoto wangu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 47:8
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitapanda juu ya mawingu nitajifanya kuwa sawa na Mungu Mukubwa.


Mutetemeke kwa woga, enyi munaojiikalia tu; mutetemeke kwa hofu, enyi munaostarehe! Muvue nguo zenu, mubakie uchi, mujifungie nguo ya gunia katika viuno vyenu.


Musimame, enyi wanawake munaostarehe, munisikilize; musikilize maneno ninayosema, enyi wabinti musiojali kitu.


Hivi ndivyo anavyosema Yawe aliyeumba mbingu, ndiye Mungu aliyeipa dunia umbo na kuifanya na kuiimarisha. Hakuiumba kusudi ibaki ukiwa, lakini aliipa umbo kusudi iikaliwe na viumbe vyake: Mimi ni Yawe, wala hakuna mwingine.


Mimi ni Yawe, wala hakuna mwingine; hakuna Mungu mwingine lakini mimi. Ninakuimarisha ingawa wewe haunijui,


kusudi watu wote, toka mashariki mpaka magaribi, wajue kwamba hakuna Mungu mwingine isipokuwa mimi tu. Mimi ni Yawe na hakuna mwingine.


Ulijiona salama katika uovu wako; ukajisemesha: Hakuna mutu anayeniona. Hekima na elimu yako vilikupotosha, ukajisemesha ndani ya moyo wako: Mimi ndiye; hakuna mwingine isipokuwa mimi.


Simama uende kulishambulia taifa linalostarehe, taifa linaloishi kwa usalama. –Ni ujumbe wa Yawe.– Taifa hilo halina milango wala vifungio vya chuma; ni taifa ambalo liko peke yake.


Enyi wanyanganyi wa mali yangu, ijapokuwa munafurahi na kushangilia, munarukaruka kama mwana-ngombe anayepepeta ngano, na kulia kama farasi dume,


Ingawa Babeli ungepanda mpaka mbinguni, na kuziimarisha kuta zake ndefu, waangamizaji watakuja kutoka kwangu kwa kuuharibu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kosa la dada yako Sodoma, lilikuwa hili: yeye pamoja na wabinti wake walipokuwa na chakula nao walifanikiwa sana, walianza kujivuna, wakaacha kuwasaidia wamasikini na wakosefu.


Wewe mwanadamu! Umwambie mufalme wa Tiro kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Wewe una kiburi cha moyo, na umesema kwamba wewe ni mungu, kwamba umeikalia kiti cha kifalme cha miungu, umekaa mbali huko katika bahari. Lakini, wewe ni mutu tu wala si mungu, ingawa unajiona kuwa na hekima kama mungu.


Siku hiyo, nitapeleka wajumbe kwenda kuwatisha Waetiopia wanaojizania kuwa na usalama. Watatetemeka siku Misri itakapoangamia. Kweli! Kweli siku hiyo inakuja!


Mufalme atafanya kama anavyopenda. Atajitukuza na kujivuna kwamba yeye ni mukubwa kuliko miungu yote, na kumutukana Mungu wa miungu. Ataendelea kufanikiwa mpaka kasirani ifikie ukomo wake, maana yaliyopangwa sherti yatimie.


Wewe utafukuzwa mbali na wanadamu. Utaishi pamoja na nyama wa pori, utakula majani kama ngombe; utalowana na umande wa mbinguni. Utakaa katika hali hiyo kwa miaka saba, na kwa mwisho utatambua kwamba Mungu Mukubwa ndiye anayetawala juu ya ufalme wa wanadamu naye anamupa ufalme ule mutu yeyote anayemutaka.


Basi, akasema kwa sauti: Angalia Babeli, muji mukubwa nilioujenga kwa nguvu zangu ukuwe makao yangu ya kifalme na kwa ajili ya utukufu wangu!


Mara moja jambo hilo juu ya mufalme Nebukadneza likatimizwa. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akakuwa anakula majani kama ngombe. Alilowanishwa na umande wa mbinguni, na nywele zake zikakuwa ndefu kama manyoya ya tai, na kucha zake kama za ndege.


Halafu waganga, walozi, Wakaldea na wenye hekima wakaletwa. Nikawaelezea ndoto yangu, lakini hawakuweza kunieleza maana yake.


Pahali pake umejitukuza mwenyewe mbele ya Bwana wa mbinguni: umeleta vyombo vya nyumba ya Mungu ukavitumia kwa kunywea divai, wewe, wakubwa wako, wanawake wako na wahabara wako, na kuisifu miungu iliyotengenezwa na feza, zahabu, shaba, chuma, miti na mawe; miungu ambayo haioni, haisikii wala haijui jambo lolote. Lakini Mungu, ambaye uzima wako uko katika mukono wake, na njia zako ziko wazi mbele yake, haukumuheshimu!


Usiku uleule, mufalme Belsasari wa Wakaldea, aliuawa.


Watateketezwa kama kichaka cha miiba, wao wanaoikalia kulewa. Watateketezwa kama vile majani yenye kukauka.


Ninawe! Wewe umekuwa kama kahaba. Umewashawishi watu, ewe binti wa uchawi, uliyeyafanya mataifa kuwa watumwa kwa ukahaba wako, na watu wa mataifa kwa uchawi wako.


Wao ni watu wa kuchukiza na kutisha; wao wanajiamulia sheria wenyewe na kujipatia mamlaka.


Basi huu ndio muji uliojivuna na kuishi kwa usalama, muji uliojisemesha: Ni mimi tu, hakuna mwingine! Jinsi gani umekuwa mutupu na makao ya nyama wa pori! Kila mutu anayepita karibu atauzomea na kuuzarau.


Yeye atapinga kitu chochote watu wanachohesabu kuwa cha kimungu au wanachoabudu na kujiweka kuwa juu ya vyote. Yeye ataenda hata kuingia katika hekalu la Mungu na kukaa mule na kujiita mwenyewe kuwa Mungu.


Hao watu wa kabila la Dani walivitwaa vitu vile ambavyo Mika alikuwa amevitengeneza, na kumupeleka yule kuhani aliyemutumikia. Basi wakaenda kushambulia muji wa Laisi, wakawaua wakaaji wake ambao waliishi mule kwa utulivu na bila wasiwasi, wakauteketeza muji ule.


Basi, watu hao watano wakaondoka, wakaenda Laisi. Waliwaona watu walioishi kule, na jinsi walivyokaa kwa usalama kama vile watu wa Sidona. Walikuwa watu watulivu wasiokuwa na wasiwasi na hawakupungukiwa mahitaji yoyote katika inchi. Walikuwa mbali na watu wa Sidona, na hawakukuwa na shuguli yoyote na watu wengine.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ