Nitakapopita, kila muzaliwa wa kwanza katika inchi ya Misri atakufa, kuanzia muzaliwa wa kwanza wako wewe mufalme wa Misri ambaye ni murizi wako, mpaka muzaliwa wa kwanza wa mujakazi anayesaga ngano kwa jiwe. Hata wazaliwa wa kwanza wa mifugo nao wote watakufa.
Basi, mufalme wa Asuria atawapeleka Wamisri na Wakushi kuwa wafungwa, wakubwa kama vile wadogo. Watapelekwa, nao watatembea uchi na bila viatu, matako wazi. Misri ipate haya!
Nawe utajiuliza hivi katika moyo wako: Kwa nini mambo haya yamenipata? Sawa! Ikiwa kanzu yako imepandishwa, na kutendewa kwa kinguvu, hayo ni matokeo ya makosa yako mengi sana.
Mataifa yote yatamutumikia yeye, pamoja na mwana wake na mujukuu wake mpaka wakati inchi yake itakapoanguka. Kisha mataifa mengi na wafalme wengi wakubwa watamufanya kuwa mutumwa wao.
Enyi wakaaji wa Safiri, muende mukiwa uchi na wenye haya. Wakaaji wa Zanana musitoke inje ya muji wenu. Watu wa Beti-Ezeli wanalia; musaada wao kwenu umeondolewa.
Lakini mwanamuke yeyote asipofunika kichwa chake wakati anapoomba au anapotabiri, anamuzaraulisha mume wake. Tendo hilo linahesabiwa kama vile amenyolewa.
Wafilistini wakamukamata, wakamwongoa macho, wakamupeleka Gaza, wakamufunga kwa minyororo ya shaba, na kumulazimisha kufanya kazi ya kusaga unga kule katika kifungo.