Isaya 47:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
12 Endelea basi na uganga wako, tegemea wingi wa uchawi wako. Wewe uliyashugulikia tangu ujana wako ukitumainia kwamba utafanikiwa au kusababisha woga kwa watu!
Watu wamoja watawaambia ninyi: Muombe shauri kwa mizimu na waaguzi wanaolia kama ndege; kwa sababu ni kawaida watu kuomba shauri kwa miungu yao, na kuomba shauri kwa wafu kwa ajili ya wanaokuwa wazima.
Lakini iko wapi ile miungu yenu muliyojifanyia? Basi kama inaweza, isimame iwasaidie, wakati munapokuwa katika shida. Ee ninyi watu wa Yuda, hesabu ya miungu yenu ni sawa na hesabu ya miji yenu!
Mufalme wa Babeli anasimama kwa mwanzo wa hizo njia mbili, kwenye masanganjia, apate kuaguza. Anatikisa mishale, anauliza shauri la sanamu ya miungu yake na kuchunguza maini ya nyama.
Ninawe! Wewe umekuwa kama kahaba. Umewashawishi watu, ewe binti wa uchawi, uliyeyafanya mataifa kuwa watumwa kwa ukahaba wako, na watu wa mataifa kwa uchawi wako.