Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 46:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Mukumbuke mambo niliyotenda hapo zamani! Mimi ni Mungu. Hakuna Mungu mwingine. Mimi ni Mungu. Hakuna mwingine kama mimi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 46:9
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata hivyo mambo haya uliyaficha ndani ya moyo. Lakini ninajua kwamba ile ilikuwa nia yako.


Amesababisha matendo yake ya ajabu yakumbukwe; Yawe ni mwenye huruma na rehema.


“Ewe Yawe, ni nani kati ya miungu anayelingana nawe? Ni nani aliyekuwa kama wewe unayekuwa mutakatifu mukubwa, unayetisha kwa matendo matukufu, unayetenda mambo ya ajabu?


Watu wakawakusanya vyura wale malundomalundo. Inchi nzima ikanuka.


Maana mara hii, wewe mwenyewe, wakubwa wako na watu wako mutapatwa na mapigo yangu makali. Nawe utatambua kwamba hakuna yeyote katika dunia anayekuwa kama mimi.


Nani aliyetangaza haya tangu mwanzo, hata sisi tupate kuyatambua? Nani aliyetangulia kuyatangaza, kusudi sasa tuseme, alisema ukweli? Hakuna hata mumoja kati yenu aliyeyataja, wala hakuna aliyesikia maneno yenu.


Mimi ni yule wa kwanza. Nilitangaza kwa Sayuni, nikapeleka Yerusalema mujumbe wa habari njema.


Mambo niliyotabiri yametukia; na sasa ninatangaza mambo mapya, ninakuelezea hayo mbele hayajatukia.


Ninyi Waisraeli ni washuhuda wangu. –Ni ujumbe wa Yawe.– Niliwachagua mukuwe watumishi wangu, mupate kunijua na kuniamini, kwamba mimi ni Mungu. Mbele yangu hakukuwa mungu mwingine, wala hakutakuwa mungu mwingine nyuma yangu.


Yawe anasema hivi: Utajiri wa Misri na faida ya uchuuzi za Kushi, pamoja na za watu wa Seba, wale watu warefu sana, zitakuja kwako mwenyewe wewe taifa la Israeli, zote zitakuwa mali yako. Watu hao watakufuata wakifungwa minyororo; watainama mbele yako na kukusihi wakisema: Kwako kuna Mungu wa kweli, wala hakuna Mungu mwingine lakini yeye.


Hivi ndivyo anavyosema Yawe aliyeumba mbingu, ndiye Mungu aliyeipa dunia umbo na kuifanya na kuiimarisha. Hakuiumba kusudi ibaki ukiwa, lakini aliipa umbo kusudi iikaliwe na viumbe vyake: Mimi ni Yawe, wala hakuna mwingine.


Mutanifananisha na nani na kunisawanisha naye? Mutanilinganisha na nani nipate kuwa sawasawa naye?


Nilitangaza zamani matukio ya mbele, niliyatangaza mimi mwenyewe na kuyafanya yajulikane kwenu. Mara moja nikaanza kuyatimiza, nayo yakapata kutukia.


Sasa, ninaumba mbingu mupya na dunia mupya. Mambo ya zamani hayatakumbukwa tena.


Kama vile simba anavyochomoka kutoka ndani ya vichaka vya muto Yordani na kuingia kwenye mbuga, ndivyo nitakavyowafukuza kwa rafla Waedomu toka katika inchi yao. Nami nitamuweka huko mutawala yeyote nitakayemuchagua. Maana, ni nani anayeweza kulinganishwa nami? Nani anayeweza kunishitaki? Ni muchungaji gani anayeweza kunipinga?


Kama vile simba anavyotoka ndani ya vichaka vya muto Yordani na kuingia kwenye mbuga, ndivyo nitakavyowafukuza kwa rafla watu wake kutoka kwake. Nami nitamuweka huko mutawala yeyote nitakayemuchagua. Maana, ni nani anayeweza kulinganishwa nami? Nani anayeweza kunishitaki? Ni muchungaji gani anayeweza kunipinga?


Yawe anasema hivi: Musimame katika masanganjia, muangalie. Muulize juu ya matukio ya zamani. Mutafute pahali panapokuwa njia nzuri muifuate, nanyi mutaweza kupumzika. Lakini wao wakasema: Hatutafuata njia hiyo.


Mutatambua kwamba mimi niko kati yenu, enyi Waisraeli; na kwamba mimi Yawe, ndimi Mungu wenu wala hakuna mwingine. Watu wangu, hawatazarauliwa tena hata kidogo.


Ingawa hivi, kwa ngambo yetu sisi tuko na Mungu mumoja peke yake tu, ndiye Baba aliyeumba vitu vyote, nasi tunaishi kwa nguvu yake. Vilevile kuko Bwana mumoja tu, ndiye Yesu Kristo. Kwa njia yake vitu vyote viliumbwa, nasi tunaishi kwa nguvu yake.


Mukumbuke siku zilizopita, mufikiri miaka ya vizazi vingi. Muulize baba zenu nao watawajulisha, muulize wakubwa wenu nao watawaelezea.


Musa akamalizia kwa kusema: “Ee Israeli, hakuna anayekuwa kama Mungu wako, yeye anayeruka toka mbinguni kuja kukusaidia, anapita juu katika anga katika utukufu wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ