Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 46:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Wanajibebesha sanamu hiyo juu ya mabega na kuipeleka, kisha wanaiweka pahali pake, nayo inakaa palepale; haiwezi hata kidogo kusogea kutoka pale inapokuwa. Mutu akiililia, haiwezi kumwitikia, wala haiwezi kumwokoa mutu katika taabu zake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 46:7
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hao manabii wakamutwaa ngombe dume wao waliyepewa, wakamutayarisha, kisha wakaanza kumulilia Bali kutokea asubui mpaka saa sita za muchana, wakirukaruka pembeni ya mazabahu waliyotengeneza wakisema: “Ee Bali, utusikilize!” Lakini hakukutokea sauti yoyote, wala hakuna aliyewajibu.


Wakaendelea kupiga makelele na kufanya kama vile wenda-wazimu mpaka nyuma ya saa sita wakati wa kutoa sadaka. Lakini hakuna aliyewajibu wala kuwajali.


Halafu Elia akawaambia: “Muwakamate manabii wote wa Bali. Musimwache hata mumoja wao atoroke!” Basi, watu wakawakamata wote, naye Elia akawapeleka kwenye muto Kisoni, akawauia kule.


Siku moja, wakati Saniharibu alipokuwa akiabudu katika nyumba ya Nisiroki mungu wake, wana wake wawili, Adarameleki na Sarezeri, walimwua kwa upanga, halafu wakakimbilia katika inchi ya Ararati. Halafu mwana wake Esari-Hadoni akatawala kwa pahali pake.


Au ni sanamu ya muti mugumu? Hiyo ni kuni mutu anayochagua, akamutafuta fundi anayeelewa kazi, naye anamuchongea sanamu imara!


Nimeangalia vizuri sana, lakini simwoni mutu yeyote; hakuna yeyote kati ya hao miungu anayeweza kushauri; nikiuliza, hakuna anayeweza kunijibu.


Miungu hiyo yote ni udanganyifu, haiwezi kufanya kitu chochote; sanamu zao ni upepo tu, hazina maana.


Fundi anamusaidia mufuaji wa zahabu. Naye anayelainisha sanamu kwa hama, anamusaidia anayeiunga kwa misumari. Wote wanasema: Ni vizuri sana! Kisha wanaifunga kwa misumari isitikisike.


Mufuaji wa vyuma anatwaa kipande cha chuma, anakiyeyusha kwa moto na kufua sanamu. Anakipondaponda na nyundo kusudi akipatie umbo kwa mikono yake yenye nguvu. Wakati wote huo yeye anasikia njaa na kuchoka; anasikia kiu na nguvu kuregea.


Enyi watu wa mataifa muliobaki, mukusanyike pamoja mukuje! Ninyi mumekosa akili: ninyi munabeba sanamu za miti na kumwomba mungu asiyeweza kuokoa watu.


Ule mungu Bali ameanguka; mungu Nebo anainama. Sanamu zao zinabebwa juu ya nyama, juu ya nyama wanaobeba mizigo! Vitu ninyi mulivyokuwa mukiviinua juu, vinakuwa sasa mizigo, vinakuwa mizigo mizito juu ya nyama wenye kuchoka.


Ndivyo watakavyokuwa hao uliowategemea hivyo, hao uliojishugulisha nao tangu ujana wako. Watatangatanga kila mumoja njia yake; hakuna hata mumoja atakayeweza kukuokoa.


Sanamu zao ni kama sanamu za kutishia ndege katika shamba la maboga, hazina uwezo wa kuongea; ni lazima zibebwe maana haziwezi kutembea. Musiziogope sanamu hizo, maana haziwezi kuzuru, wala haziwezi kutenda jambo lolote jema.


Kwa hiyo wakaaji wa Yuda na wa Yerusalema watakapoiendea miungu yao ambayo wanaifukizia ubani, lakini miungu hiyo haitaweza kuwaokoa wakati huo wa hasara itakayowapata.


Lakini iko wapi ile miungu yenu muliyojifanyia? Basi kama inaweza, isimame iwasaidie, wakati munapokuwa katika shida. Ee ninyi watu wa Yuda, hesabu ya miungu yenu ni sawa na hesabu ya miji yenu!


Mufalme Nebukadneza alitengeneza sanamu ya zahabu, yenye urefu wa metre makumi mbili na nane na upana wa metre tatu. Akaisimamisha katika bonde la Dura katika jimbo la Babeli.


Watumishi wa mashua wakaogopa, kila mumoja akaanza kumulilia mungu wake. Wakatupa katika bahari mizigo yote kwa kupunguza uzito wa mashua. Wakati ule, Yona alikuwa ameshuka katika sehemu ya ndani ya mashua, akalala usingizi muzito.


Munajua kwamba wakati mulipokuwa wapagani, mulikuwa mukivutwa na kupotoshwa na sanamu zisizosema.


Kesho yake asubui, watu wa muji wa Asidodi walipoamuka waliona sanamu ya Dagoni imeanguka ikilalia uso chini mbele ya Sanduku la Mungu. Wakaisimamisha tena sanamu ya Dagoni na kuiweka tena pahali pake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ