Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 46:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Mimi nitabaki yuleyule hata katika uzee wenu; hata katika wakati wenu wa imvi mimi nitawabeba. Nilifanya hivyo kwanza, nitafanya hivyo tena. Nitawabeba ninyi na kuwaokoa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 46:4
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Muangalie kuta zake na kuchunguza pango zake za kukimbilia, mupate kuelezea vizazi vitakavyokuja kwamba:


Anapanda juu akichukua wafungwa, anapokea zawadi kutoka kwa watu, hata kutoka kwa watu walioasi, Yawe apate kukaa huko.


Usiniachilie, ee Mungu, nitakapokuwa muzee mwenye imvi nyingi, kusudi nivitangazie vizazi vitakavyokuja nguvu yako.


Wakati wa uzee usinitupe; ninapoishiwa na nguvu usiniachilie.


Kama miti iliyopandwa katika nyumba ya Yawe, wanastawi katika viwanja vya Mungu wetu;


Nani aliyefanya yote haya yatendeke? Ni nani aliyepanga wakati wa kila tukio? Mimi Yawe nipo tangu mwanzo, mimi nitakuwa hata milele.


Mimi ni Mungu na nitakuwa Mungu siku zote. Hakuna anayeweza kuepuka nguvu yangu; hakuna anayeweza kupinga ninayofanya.


Lakini mimi ndiye niliyefuta makosa yenu kwa heshima yangu, ndiye ninayefuta makosa kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka zambi zenu.


Unisikilize ee taifa la Yakobo, unisikilize ee Israeli niliyekuita. Mimi ndiye. Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.


Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Ninachukia kuachana. Ninachukia wakati mumoja wenu anapomutendea muke wake ubaya ule. Muhakikishe kwamba hakuna hata mumoja wenu anayekosa uaminifu kwa muke wake.


Yawe wa majeshi alisema hivi: Mimi Yawe sibadiliki. Ni kwa sababu hii, ee ninyi wazao wa Yakobo, hamujateketezwa.


Kwa maana Mungu habadilishi mafikiri juu ya zawadi anazotoa, wala juu ya wale anaowachagua.


kule katika jangwa ambako muliona jinsi alivyowabeba safari hiyo yote kama vile baba anavyobeba mwana wake, mpaka mukafika hapa.


Utavikunjakunja kama kanzu, navyo vitabadilishwa kama nguo. Lakini wewe utabaki sawasawa, na maisha yako hayatakuwa na mwisho.”


Yesu Kristo ni yule yule, jana, leo na hata milele.


Kila zawadi nzuri na kila zawadi kamilifu inatoka juu kwa Mungu Baba aliyeumba miangaza yote inayokuwa katika mbingu. Mungu hawezi kubadilika wala kugeuka.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ