Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 46:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ule mungu Bali ameanguka; mungu Nebo anainama. Sanamu zao zinabebwa juu ya nyama, juu ya nyama wanaobeba mizigo! Vitu ninyi mulivyokuwa mukiviinua juu, vinakuwa sasa mizigo, vinakuwa mizigo mizito juu ya nyama wenye kuchoka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 46:1
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Utamutegemea kwa sababu ana nguvu nyingi na kumwacha akufanyie kazi zako nzito?


“Usiku ule, nitapita katika inchi ya Misri na kuwaua wazaliwa wa kwanza wa Misri, watu na nyama. Nitaiazibu miungu yote ya Misri. Mimi ni Yawe.


Siku hiyo, watu watawatupia panya na popo sanamu za feza na zahabu walizojitengenezea kusudi waziabudu.


Angalia, wanakuja: waaskari wapanda-farasi wawiliwawili. Wanasema: Babeli umeanguka! Umeanguka! Sanamu zote za miungu yake zimetupwa chini na kuvunjwavunjwa!


Ujumbe wa Mungu juu ya nyama wa pande za jangwa ya kusini: Wajumbe wanapita katika inchi ya taabu na shida, yenye simba, nyoka wa sumu na nyoka wakubwa wanaoruka. Wamewabebesha punda na ngamia wao mali zao, kuwapelekea watu wasioweza kuwafalia kitu.


Enyi watu wa mataifa muliobaki, mukusanyike pamoja mukuje! Ninyi mumekosa akili: ninyi munabeba sanamu za miti na kumwomba mungu asiyeweza kuokoa watu.


Wanajibebesha sanamu hiyo juu ya mabega na kuipeleka, kisha wanaiweka pahali pake, nayo inakaa palepale; haiwezi hata kidogo kusogea kutoka pale inapokuwa. Mutu akiililia, haiwezi kumwitikia, wala haiwezi kumwokoa mutu katika taabu zake.


Sanamu zao ni kama sanamu za kutishia ndege katika shamba la maboga, hazina uwezo wa kuongea; ni lazima zibebwe maana haziwezi kutembea. Musiziogope sanamu hizo, maana haziwezi kuzuru, wala haziwezi kutenda jambo lolote jema.


Mutangaze kati ya mataifa, munyanyue bendera na kutangaza, musifiche jambo lolote. Museme: Babeli umetekwa, mungu Beli amepatishwa haya. Merodaki amefazaishwa; sanamu zake zimefezeheshwa, miungu yake imefazaishwa.


Jua kali liyapige maji, kusudi yapate kukauka! Maana Babeli ni inchi inayojaa sanamu za miungu, watu ni wenda-wazimu kwa sababu ya miungu yao.


Nitamwazibu mungu Beli huko Babeli, nitamutapikisha kile alichomeza. Mataifa hayatamwendea tena kwa wingi. Ukuta wa Babeli umebomoka.


Kwa hiyo, siku zinakuja ambapo nitaazibu sanamu za Babeli; inchi yake yote itapata haya, watu wake wote watauawa humohumo. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Kwa hiyo, siku zinakuja ambapo nitaiazibu miungu ya Babeli, na wenye kuumizwa watalalamika katika inchi yake yote. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Atabeba sanamu za miungu yao na vyombo vya bei kali vya feza na zahabu mpaka katika inchi ya Misri. Kwa muda wa miaka michache, mufalme wa kusini hatamushambulia mufalme wa kaskazini.


Mufalme Nebukadneza akawauliza: Ni kweli kwamba wewe Sadiraki, wewe Mesaki na wewe Abedenego, hamwitumikii miungu yangu wala kuiabudu ile sanamu ya zahabu niliyoisimamisha?


Yawe ameamuru hivi juu ya Ninawe: Hautapata wazao kwa kulidumisha jina lako. Sanamu zako za kuchonga na za chuma chenye kuyeyushwa, nitazivunjavunja katika nyumba za miungu yako. Mimi nitakuchimbia kaburi lako, maana wewe haufai kwa kitu chochote.


Nebo na Bali-Meoni (majina ya hiyo miji yalibadilishwa), na Sibuma. Miji waliyoijenga wakaipa majina mengine.


Wanafunga mizigo mizito na kuibebesha watu wengine kwa mabega, lakini wao wenyewe hawafikiri hata kidogo juu ya namna ya kuwasaidia kuibeba.


Kesho yake asubui, watu wa muji wa Asidodi walipoamuka waliona sanamu ya Dagoni imeanguka ikilalia uso chini mbele ya Sanduku la Mungu. Wakaisimamisha tena sanamu ya Dagoni na kuiweka tena pahali pake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ