Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 45:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Nitakupa akiba zilizofichwa na mali inayokuwa pahali pa siri, upate kutambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wa Israeli, ninayekuita kwa jina lako.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 45:3
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sasa, ee Yawe, Mungu wa Israeli, ninakusihi utimize yote uliyomwahidi mutumishi wako Daudi.


Hivi ndivyo Kiro mufalme wa Persia anavyosema: Yawe, Mungu wa mbingu, amenipatia falme zote katika ulimwengu na ameniagiza nimujengee nyumba katika Yerusalema, huko Yuda.


Musa akamwambia Yawe: Wewe unaniambia: Uwaongoze watu hawa, lakini haujanijulisha ni nani utakayemutuma anisaidie. Hata hivyo umesema kwamba unanijua kwa jina langu na vilevile kwamba nimepata kukubaliwa mbele yako.


Yawe akamwambia Musa: Kwa sababu umepata kukubaliwa mbele yangu, nami ninakujua kwa jina lako, jambo hilihili ulilolisema nitalifanya.


Mutuambie yatakayotokea nyuma, nasi tujue basi kama ninyi ni miungu. Mufanye kitu chochote, chema au kibaya, kusudi tushangae na kuogopa.


Yawe aliyewaumba enyi watu wa Yakobo, yeye aliyewafanya enyi watu wa Israeli, anasema hivi: Musiogope, maana mimi nimewakomboa; nimewaita kwa jina lenu nanyi ni wangu.


Mimi –ni mimi!– nimesema na kumwita; nimemuleta, naye atafanikiwa katika mupango wake.


Munisikilize, enyi inchi za mbali, Mutege sikio, enyi watu wa mbali! Yawe aliniita mbele sijazaliwa, alitaja jina langu nikiwa katika tumbo la mama yangu.


Lakini kulikuwa watu kumi katika kundi hilo waliomwambia Isimaeli hivi: Tafazali usituue, maana tuna akiba kubwa ya ngano, shayiri, mafuta na asali ambayo tumeificha katika pori. Basi hao akawaacha wazima.


Mukuje kumushambulia kutoka kila upande; muzifungue gala zake za chakula; mumulundikie malundo ya ngano! Muiangamize kabisa inchi hii; musiache kitu chochote!


Upanga ukuwe juu ya farasi wake na magari yake, juu ya majeshi yake yote ya mushahara, kusudi wakuwe sawa na wanawake! Upanga ukuwe juu ya hazina zake zote kusudi zinyanganywe.


Inchi hiyo imejaa mito na akiba tele, lakini mwisho wake umefika, uzi wa uzima wake umekatwa.


Ingawa Babeli ungepanda mpaka mbinguni, na kuziimarisha kuta zake ndefu, waangamizaji watakuja kutoka kwangu kwa kuuharibu. –Ni ujumbe wa Yawe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ