Wewe ndiwe Mungu wetu! Uwaazibu, maana sisi hatuna uwezo wowote mbele ya jeshi kubwa kama hili linalotufikia. Hatujui la kufanya lakini tunatazamia musaada kutoka kwako.”
Bwana wetu Yawe, Mutakatifu wa Israeli anasema hivi: Mukinirudilia na kutulia mutaokolewa; kwa utulivu na kunitumainia mutapata nguvu. Lakini ninyi hamukutaka.
Mujongee, mutuambie yatakayotukia. Mutuambie matukio ya kwanza yalikuwa gani, nasi tutafikiri juu yake. Au mututangazie jinsi yatakavyotimia, kusudi tujue yatakayokuja.
Mutangaze na kusema habari zenu. Mufanye shauri pamoja! Ni nani aliyetangaza zamani matukio ya sasa? Ni nani aliyesema mambo haya zamani? Haikukuwa mimi Yawe? Hakuna Mungu mwingine isipokuwa mimi! Mimi ni Mungu wa haki na mwokozi; hakuna mwingine isipokuwa mimi.
Yeye anasema: Haitoshi tu wewe kuwa mutumishi wangu, kusudi uyainue makabila ya Yakobo, na kurudisha watu wa Israeli waliobaki. Nitakufanya ukuwe mwangaza wa mataifa, kusudi watu wote wapate kuokolewa katika dunia.
Sasa utayaita mataifa usiyoyajua, watu wa mataifa yasiyokutambua watakuja mbio kwenu, kwa sababu yangu mimi Yawe, Mungu wako; kwa sababu yangu mimi Mutakatifu wa Israeli niliyekufanya wewe upate utukufu.
Yeye ndiye atakayeleta amani. Waasuria wakishambulia inchi yetu, na kuingia katika nyumba zetu nzuri, tutatuma walinzi wetu wapigane nao, tutawapeleka waongozi wetu kwa wingi.
Halafu nitawajaza wazao wa Daudi na wakaaji wa muji Yerusalema roho ya huruma na maombi, nao watamwangalia yule waliyemutoboa kwa mukuki; watamulilia kama vile mutu anavyolia kwa kifo cha mutoto wake wa pekee, au kama vile mutu anavyomulilia kwa uchungu muzaliwa wake wa kwanza.
Tukaze macho yetu kuelekea Yesu mwenye kuanzisha na kukamilisha imani yetu. Kwa sababu alijua furaha atakayopata nyuma, alivumilia kufa juu ya musalaba pasipo kuona haya, na sasa anaikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu kwenye kiti cha kifalme cha Mungu.
Barua hii inatoka kwangu mimi Simoni Petro, mutumishi na mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi mulioshiriki pamoja nasi katika imani ile inayokuwa kubwa kwa njia ya haki ya Mungu wetu na Mwokozi Yesu Kristo.