Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 45:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Ni mimi niliyemwamuru Kiro akuje, atimize mapenzi yangu. Nitazifanikisha njia zake zote. Ataujenga upya muji wangu Yerusalema, na kuwapa uhuru watu wangu wanaokuwa katika uhamisho, bila kutaka malipo wala zawadi. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 45:13
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi sasa, kila mutu kati yenu ninyi wote munaokuwa watu wake, Mungu wake akuwe naye na aende katika Yerusalema huko Yuda, na kuijenga upya nyumba ya Yawe, Mungu wa Israeli, Mungu anayeabudiwa kule Yerusalema.


Heri wale unaowachagua na kuwaleta karibu, waishi katika kiwanja chako. Sisi tutatoshelewa na mazuri ya nyumba yako, mazuri ya hekalu lako takatifu.


Umutambue Mungu katika kila kitu unachofanya, naye atasawanisha njia zako.


Ninawachochea Wamedi juu yao; watu ambao hawajali feza wala hawavutwi na zahabu.


aliyegeuza dunia kuwa kama jangwa, akaangamiza miji yake, na kukataa kuwafungua wafungwa wake?


Ni nani aliyemwita shujaa toka mashariki, mutu ambaye anapata ushindi popote anapoenda? Mimi ninayaweka mataifa katika mikono yake, naye anawaponda wafalme chini ya miguu yake! Upanga wake unawafanya kuwa kama mavumbi, kwa upinde wake anawapeperusha kama maganda.


Nimetokeza mutu toka kaskazini, naye amekuja; nimemuchagua mutu toka mashariki, naye atalitaja jina langu. Yeye atawakanyaga wafalme kama matope, kama vile mufinyanzi anavyoponda udongo wake.


Mimi Yawe nimekuita kutenda haki, nimekushika mukono na kukulinda. Kwa njia yako nitafanya ahadi na watu wote, wewe utakuwa mwangaza wa mataifa.


Ndimi ninasema juu ya mufalme Kiro: Ni muchungaji niliyemuchagua kwa ajili yangu. Yeye atatimiza mipango yangu yote. Ndimi ninayesema juu ya Yerusalema: Wewe Yerusalema utajengwa tena upya; na juu ya hekalu: Musingi wako utawekwa tena.


Mimi nitakutangulia, na kuisawanisha milima mbele yako. Nitaivunjavunja milango ya shaba, na kuvikatakata vifungio vyake vya chuma.


Ninamwita tai wangu kutoka mashariki, ambaye atatimiza kusudi langu toka inchi ya mbali. Mimi nimesema na nitafanya; mimi nimepanga nami nitatimiza.


Yawe anasema hivi: Kweli! Hata mateka za shujaa zitarudishwa, wafungwa wa mutu mutesaji wataokolewa. Mimi mwenyewe nitawapiganisha waadui zako, mimi mwenyewe nitawaokoa watoto wako.


Katika hali ya sasa ninapata faida gani kuwaona watu wangu wamepelekwa katika utumwa? –Ni ujumbe wa Yawe. Hao wanaowatawala wanajitapa. Nalo jina langu linaendelea kuzarauliwa kila siku. –Ni ujumbe wa Yawe.


Enyi watu wa Sayuni, mulie na kugaagaa kama mwanamuke anayezaa! Maana sasa mutaondoka katika muji huu muende kukaa katika mbuga, mutakwenda mpaka Babeli. Lakini kule, mutaokolewa. Kule Yawe atawakomboa toka katika makucha ya waadui zenu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ