Isaya 44:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
3 Nitaimwangilia maji inchi yenye kiu, na kutiririsha muto katika inchi iliyokauka. Nitajaza roho wangu juu ya wazao wako, nitawamwangia watoto wako baraka yangu.
Hali itaendelea kuwa hivyo mpaka tujazwe Roho wa Mungu kutoka juu. Hapo jangwa litakuwa shamba lenye udongo muzuri tena, na mashamba yenye udongo muzuri yatakuwa pori.
Kila mumoja atakuwa kama pahali pa kujikinga na upepo, kama pahali pa kujificha wakati wa mvua kubwa. Watakuwa kama vijito vya maji katika inchi yenye kukauka, kama kivuli cha jiwe kubwa katika jangwa.
Hawatasikia tena njaa wala kuwa na kiu. Upepo wenye kuunguza wala jua havitawachoma, mimi niliyewahurumia nitawaongoza na kuwapeleka kwenye chemichemi za maji.
Ee ninyi wote wenye kiu mukuje kwenye maji! Mukuje, wote hata musiokuwa na feza; mununue chakula na mupate kula, mununue divai na maziwa. Bila feza, bila malipo!
Yawe anasema: Mimi ninafanya nanyi agano hili: Roho wangu anayekuwa juu yenu, maneno niliyoyaweka katika kinywa chenu, hayataondoka kwenu hata kidogo, wala kwa watoto na wajukuu wenu, tangu sasa na hata milele.
Akaniambia: Maji haya yanatiririka kupitia katika inchi mpaka katika bonde la Yordani, na yakifika huko yatayafanya maji ya bahari ya Chumvi kuwa maji mazuri.
Mutatambua kwamba mimi niko kati yenu, enyi Waisraeli; na kwamba mimi Yawe, ndimi Mungu wenu wala hakuna mwingine. Watu wangu, hawatazarauliwa tena hata kidogo.
Kisha mambo hayo nitashusha Roho wangu juu ya watu wote. Watoto wenu wanaume na wabinti watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono.
Wazao wa Yakobo watakaobaki wazima, wataenea kati ya mataifa na watu wengi watakuwa na nguvu kubwa kama simba kati ya nyama wa pori, kama simba mukali kati ya makundi ya kondoo, ambaye kila pahali anapopita, anarukia na kurarua nyama, na hakuna mutu yeyote wa kuiokoa.
Halafu nitawajaza wazao wa Daudi na wakaaji wa muji Yerusalema roho ya huruma na maombi, nao watamwangalia yule waliyemutoboa kwa mukuki; watamulilia kama vile mutu anavyolia kwa kifo cha mutoto wake wa pekee, au kama vile mutu anavyomulilia kwa uchungu muzaliwa wake wa kwanza.
Na wale wanafunzi Wayuda waliofika pamoja na Petro wakashangaa sana kwa kuona kwamba Mungu ametoa zawadi ya Roho wake Mutakatifu kwa watu wa mataifa mengine vilevile.
‘Mungu anasema: Katika siku za mwisho, nitashusha Roho wangu juu ya watu wote; wana wenu na wabinti zenu watatabiri, vijana wenu wataona maono nao wazee wenu wataota ndoto.
Na kisha kunyanyuliwa aikae na mamlaka kwa kuume kwa Mungu Baba yake, yeye akamupa Roho Mutakatifu aliyeahidiwa. Naye akamushusha juu yetu, sawa vile munavyojionea na kusikia wenyewe.
Akasema tena: “Sasa ni mwisho! Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho. Yule anayesikia kiu, nitamupa maji ya kunywa yanayotoka katika chemichemi ya maji ya uzima pasipo kulipa.
Roho na Bibi arusi wanasema: “Kuja!” Naye mwenye kusikia maneno haya aseme vilevile: “Kuja!” Yule anayesikia kiu akuje, na yule anayetaka maji ya uzima akuje kuyapokea kwa bure.