Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 44:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Nitaimwangilia maji inchi yenye kiu, na kutiririsha muto katika inchi iliyokauka. Nitajaza roho wangu juu ya wazao wako, nitawamwangia watoto wako baraka yangu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 44:3
38 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Utaona vilevile wazao wako watakuwa wengi, wengi kama majani katika mashamba.


Aligeuza jangwa kuwa ziwa, na inchi ya kukauka kuwa chemichemi za maji.


Zaburi ya Daudi wakati alipokuwa katika jangwa la Yudea.


Musikilize maonyo yangu; nitawamiminia mawazo yangu, nitawajulisha maneno yangu.


Mimi, Yawe, ni mulimaji wake; ninalimwangilia maji kila wakati. Ninalilinda usiku na muchana, kusudi lisiharibiwe na mutu yeyote.


Hali itaendelea kuwa hivyo mpaka tujazwe Roho wa Mungu kutoka juu. Hapo jangwa litakuwa shamba lenye udongo muzuri tena, na mashamba yenye udongo muzuri yatakuwa pori.


Kila mumoja atakuwa kama pahali pa kujikinga na upepo, kama pahali pa kujificha wakati wa mvua kubwa. Watakuwa kama vijito vya maji katika inchi yenye kukauka, kama kivuli cha jiwe kubwa katika jangwa.


Wamasikini na wakosefu wakitafuta maji lakini hawayapati, wakiwa wamekauka koo kwa kiu, mimi Yawe nitawajibu; mimi Mungu wa Israeli, sitawaacha.


Wazao wako wangekuwa wengi kama muchanga, kama chembe za muchanga. Jina lao lisingalisahauliwa hata kidogo, wala halingalifutwa mbele yangu.


Alipowaongoza katika jangwa hawakuona kiu, aliwatiririshia maji kutoka katika jiwe, alipasua jiwe maji yakabubujika.


Hawatasikia tena njaa wala kuwa na kiu. Upepo wenye kuunguza wala jua havitawachoma, mimi niliyewahurumia nitawaongoza na kuwapeleka kwenye chemichemi za maji.


Ee ninyi wote wenye kiu mukuje kwenye maji! Mukuje, wote hata musiokuwa na feza; mununue chakula na mupate kula, mununue divai na maziwa. Bila feza, bila malipo!


Yawe anasema: Mimi ninafanya nanyi agano hili: Roho wangu anayekuwa juu yenu, maneno niliyoyaweka katika kinywa chenu, hayataondoka kwenu hata kidogo, wala kwa watoto na wajukuu wenu, tangu sasa na hata milele.


Wazao wao watajulikana kati ya mataifa; watajulikana kati ya watu wengine. Kila mutu atakayewaona atakubali kwamba wao ni watu waliobarikiwa na Yawe.


Kazi zao hazitakuwa bure, wala hawatazaa watoto watakaopatwa na musiba; maana watakuwa waliobarikiwa na Yawe, wamebarikiwa wao pamoja na wazao wao.


Nitawafanya waishi kandokando ya mulima wangu mutakatifu na kuwabariki. Nitawaletea mvua kwa wakati wake, nazo zitakuwa mvua za baraka.


Nitatia roho yangu ndani yenu; nitawafanya mufuate masharti yangu na kushika maagizo yangu.


Nitakapowajaza Waisraeli Roho yangu, sitageuka tena wasipate kuniona. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Akaniambia: Maji haya yanatiririka kupitia katika inchi mpaka katika bonde la Yordani, na yakifika huko yatayafanya maji ya bahari ya Chumvi kuwa maji mazuri.


Mupande haki kwa faida yenu, nanyi mutavuna wema; mulime mashamba yaliyoachwa, maana wakati wa kutafuta Yawe umefika kusudi awanyeshee haki kama mvua.


Mutatambua kwamba mimi niko kati yenu, enyi Waisraeli; na kwamba mimi Yawe, ndimi Mungu wenu wala hakuna mwingine. Watu wangu, hawatazarauliwa tena hata kidogo.


Kisha mambo hayo nitashusha Roho wangu juu ya watu wote. Watoto wenu wanaume na wabinti watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono.


Wazao wa Yakobo watakaobaki wazima, wataenea kati ya mataifa na watu wengi watakuwa na nguvu kubwa kama simba kati ya nyama wa pori, kama simba mukali kati ya makundi ya kondoo, ambaye kila pahali anapopita, anarukia na kurarua nyama, na hakuna mutu yeyote wa kuiokoa.


Halafu nitawajaza wazao wa Daudi na wakaaji wa muji Yerusalema roho ya huruma na maombi, nao watamwangalia yule waliyemutoboa kwa mukuki; watamulilia kama vile mutu anavyolia kwa kifo cha mutoto wake wa pekee, au kama vile mutu anavyomulilia kwa uchungu muzaliwa wake wa kwanza.


“Wakati pepo imekwisha kutoka ndani ya mutu, inazungukazunguka katika jangwa kutafuta nafasi ya kupumzikia. Naye asipopata nafasi ile,


Na wale wanafunzi Wayuda waliofika pamoja na Petro wakashangaa sana kwa kuona kwamba Mungu ametoa zawadi ya Roho wake Mutakatifu kwa watu wa mataifa mengine vilevile.


‘Mungu anasema: Katika siku za mwisho, nitashusha Roho wangu juu ya watu wote; wana wenu na wabinti zenu watatabiri, vijana wenu wataona maono nao wazee wenu wataota ndoto.


Na kisha kunyanyuliwa aikae na mamlaka kwa kuume kwa Mungu Baba yake, yeye akamupa Roho Mutakatifu aliyeahidiwa. Naye akamushusha juu yetu, sawa vile munavyojionea na kusikia wenyewe.


Kwa maana ahadi hii ya Mungu ilitolewa kwenu, kwa watoto wenu na kwa wote wanaokaa mbali, ndio wote ambao Bwana Mungu wetu atakaowaita.”


Akasema tena: “Sasa ni mwisho! Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho. Yule anayesikia kiu, nitamupa maji ya kunywa yanayotoka katika chemichemi ya maji ya uzima pasipo kulipa.


Roho na Bibi arusi wanasema: “Kuja!” Naye mwenye kusikia maneno haya aseme vilevile: “Kuja!” Yule anayesikia kiu akuje, na yule anayetaka maji ya uzima akuje kuyapokea kwa bure.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ