Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 43:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Lakini mimi ndiye niliyefuta makosa yenu kwa heshima yangu, ndiye ninayefuta makosa kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka zambi zenu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 43:25
37 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sikia maombi yangu mimi mutumishi wako na ya watu wako Waisraeli wanapoomba wakielekea pahali hapa. Usikilize maombi kutokea kule mbinguni na ukisha kusikia, usamehe.


Kama mashariki inavyokuwa mbali na magaribi, ndivyo anavyotenga zambi zetu mbali nasi.


Ananisamehe uovu wangu wote, na kuniponyesha magonjwa yote.


Kwa ajili ya jina lako, ee Yawe, unisamehe kosa langu, kwa maana ni kubwa.


Usikumbuke zambi na makosa ya ujana wangu; unikumbuke kwa kadiri ya wema wako, kwa ajili ya uzuri wako, ee Yawe.


Unihurumie, ee Mungu, kadiri ya wema wako; uyafute makosa yangu, kadiri ya wingi wa rehema yako.


Unisafishe kabisa kosa langu; unitakase zambi yangu.


Unitakase kwa hisopo, nikuwe safi, unisafishe, nikuwe mweupe pee.


Yawe anasema hivi: Mukuje basi, tukate shauri. Zambi zenu zikionekana kuwa nyekundu, zitakuwa nyeupe kama teluji; zikionekana kuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama sufu.


Nilipata mateso makali kwa faida yangu; lakini umeyaokoa maisha yangu kutoka shimo la uharibifu, maana umezitupa zambi zangu nyuma yako.


Mimi peke yangu ndiye Yawe, hakuna mukombozi mwingine isipokuwa mimi.


Nimezimisha makosa yako nayo yametoweka kama mawingu, nimefuta zambi zako, nazo zimepotea kama kunguku. Urudi kwangu maana mimi nimekukomboa.


Ninafanya hivyo kwa ajili yangu mwenyewe. Kwa nini jina langu lizarauliwe? Siwezi kumupatia mwingine utukufu wangu!


Waovu waache njia zao mbaya, watu wabaya waachane na mawazo yao mabaya; wamurudilie Yawe apate kuwahurumia, wamwendee Mungu wetu maana atawasamehe.


Usitukasirikie sana, ee Yawe, usiukumbuke uovu wetu siku zote! Ukumbuke kwamba sisi wote ni watu wako!


Miji yako mitakatifu imekuwa jangwa; Sayuni umekuwa matongo, Yerusalema umekuwa uharibifu.


Wala hawatafundishana tena kila mutu na jirani yake, na kila mutu na ndugu yake na kusema “Mumujue Yawe”, kwa sababu wote, wadogo kama vile wakubwa, watanijua mimi Mungu. Maana nitawasamehe makosa yao, wala sitazikumbuka tena zambi zao.


Siku hizo na wakati huo, uovu utatafutiwa katika inchi ya Israeli, lakini hautapatikana; zambi itatafutiwa katika inchi ya Yuda, lakini haitapatikana; maana mimi nitawasamehe wale ambao nimewaponyesha. –Ni ujumbe wa Yawe.


Makosa yake yote aliyofanya hayatakumbukwa; kwa sababu ya haki yake ataishi.


Lakini nilijizuiza kufanya hivyo kwa heshima ya jina langu kusudi lisizarauliwe kati ya watu wa mataifa ambao waliona jinsi nilivyowatoa Waisraeli katika inchi ya Misri.


Lakini nilizuiza mukono wangu kwa sababu ya heshima ya jina langu kusudi nisizarauliwe kati ya watu wa mataifa walioona nikiwatoa katika inchi ya Misri.


Lakini nilijizuiza kufanya hivyo kwa heshima ya jina langu kusudi lisizarauliwe kati ya watu wa mataifa wanaoishi nao, hao walioona nikijijulisha kwa Waisraeli wakati wa kuwatoa katika inchi ya Misri.


Zambi zake zote alizotenda hapo mbele hazitakumbukwa; yeye ametenda mambo yanayokuwa ya haki na mema, kwa hiyo hakika ataishi.


Basi, uwaambie Waisraeli kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninachotaka kufanya si kwa faida yenu ninyi watu wa inchi ya Israeli, lakini ni kwa heshima ya jina langu takatifu mulilolikufuru kati ya mataifa mulikokwenda.


Lakini mujue kwamba sitafanya hivyo kwa ajili yenu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Lakini mupate haya na kufazaika kwa sababu ya matendo yenu, enyi Waisraeli!


“Namna gani mutu huyu anasubutu kumutukana Mungu? Ni nani anayeweza kusamehe zambi isipokuwa Mungu peke yake?”


Walimu wa Sheria na Wafarisayo wakaanza kujiuliza: “Ni mutu gani huyu anayemutukana Mungu? Ni nani anayeweza kusamehe zambi, isipokuwa Mungu peke yake?”


Basi mugeuke toka katika zambi, mumurudilie Mungu, kusudi awasamehe zambi zenu.


Sheria ilitokea na kusababisha kuongezeka kwa makosa, lakini nafasi yoyote palipozidi zambi, neema ilizidi sana.


Basi tumusifu Mungu kwa sababu ya utukufu wa neema yake aliyotujalia kwa njia ya Mwana wake mupendwa.


Naye anaongeza kusema: “Nami sitakumbuka tena zambi wala maovu yao.”


Mimi nitawasamehe maovu yao, wala sitakumbuka tena zambi zao.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ