Isaya 43:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
20 Nyama wa pori wataniheshimu, mbweha na mbuni, maana nitaweka maji katika mbuga, na kububujisha mito katika jangwa, kwa kuwakunywesha watu wangu niliojichagulia,
Kila mumoja atakuwa kama pahali pa kujikinga na upepo, kama pahali pa kujificha wakati wa mvua kubwa. Watakuwa kama vijito vya maji katika inchi yenye kukauka, kama kivuli cha jiwe kubwa katika jangwa.
Muchanga wa moto katika jangwa utakuwa ziwa la maji, inchi kavu itabubujika vijito. Makao ya imbwa wa pori yatajaa maji; nyasi zitaota na kukomaa kama mianzi.
Hawatasikia tena njaa wala kuwa na kiu. Upepo wenye kuunguza wala jua havitawachoma, mimi niliyewahurumia nitawaongoza na kuwapeleka kwenye chemichemi za maji.
Watarudi wakiwa wanatoa machozi, nami nitawaongoza nikiwafariji; nitawapitisha kando ya vijito vya maji, katika njia iliyonyooka ambamo hawatajikwaa; maana mimi nimekuwa baba wa Israeli, Efuraimu ni muzaliwa wangu wa kwanza.
Na kama Bwana asingepunguza siku zile za mateso, hakuna hata mutu mumoja ambaye angeponyoka kufa. Lakini kwa ajili ya wachaguliwa aliowachagua amezipunguza.
Yesu akamujibu: “Kama ungejua kitu Mungu anachoweza kukupatia, na ni nani anayekuomba maji ya kunywa, wewe ndiwe ungemwomba, naye angekupa maji ya uzima.”
lakini yeyote atakayekunywa maji yale nitakayomupa, hatasikia kiu tena hata kidogo. Maji nitakayomupa yatakuwa ndani yake kama chemichemi inayotiririka maji ya uzima wa milele.”
Lakini ninyi ni watu wa kizazi kilichochaguliwa na Mungu na wa ukuhani wa kifalme. Ninyi ni taifa takatifu na watu wa pekee wa Mungu. Mumechaguliwa kusudi mutangaze matendo makubwa ya yule aliyewaita kutoka katika giza na kuwaingiza kwenye mwangaza wake wa ajabu.
Watapigana vita na Mwana-Kondoo, lakini Mwana-Kondoo pamoja na waaminifu wake aliowaita na kujichagulia atawashinda, kwa sababu yeye ni Bwana wa wabwana na Mufalme wa wafalme.”
Akasema tena: “Sasa ni mwisho! Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho. Yule anayesikia kiu, nitamupa maji ya kunywa yanayotoka katika chemichemi ya maji ya uzima pasipo kulipa.
Roho na Bibi arusi wanasema: “Kuja!” Naye mwenye kusikia maneno haya aseme vilevile: “Kuja!” Yule anayesikia kiu akuje, na yule anayetaka maji ya uzima akuje kuyapokea kwa bure.