Isaya 43:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
19 Muangalie, mimi ninafanya kitu kipya. Kinafanyika sasa hivi, nanyi mutaweza kukiona. Nitafanya njia katika mbuga, na kububujisha mito katika jangwa.
Angalia mimi nitasimama mbele yako juu ya jiwe la mulima wa Horebu, nawe utapiga lile jiwe na maji yatabubujika kutoka mule kusudi watu wote wapate kunywa.” Basi, Musa akafanya hivyo mbele ya wazee wa Waisraeli.
Kila mumoja atakuwa kama pahali pa kujikinga na upepo, kama pahali pa kujificha wakati wa mvua kubwa. Watakuwa kama vijito vya maji katika inchi yenye kukauka, kama kivuli cha jiwe kubwa katika jangwa.
Kwa hiyo nilikutangazia mambo yale tangu zamani, mbele hayajatukia, mimi nilikujulisha, kusudi usiseme: Ni sanamu yangu iliyotenda mambo hayo, sanamu zangu za chuma ndizo ziliyaagiza.
Hawatasikia tena njaa wala kuwa na kiu. Upepo wenye kuunguza wala jua havitawachoma, mimi niliyewahurumia nitawaongoza na kuwapeleka kwenye chemichemi za maji.
Mimi Yawe nitaufariji Sayuni, nitatengeneza pahali pake pote palipoharibika. Nitazifanya mbuga zake kama shamba la Edeni, jangwa yake kama bustani ya Yawe. Ndani yake kutapatikana furaha na shangwe, na nyimbo za shukrani zitasikilika humo.
Kwa hiyo, siku zinakuja siku ambapo watu hawataapa tena, wakisema: Kama vile Yawe anavyoishi, yule aliyewaondoa watu wa Israeli kutoka katika inchi ya Misri.
Watarudi wakiwa wanatoa machozi, nami nitawaongoza nikiwafariji; nitawapitisha kando ya vijito vya maji, katika njia iliyonyooka ambamo hawatajikwaa; maana mimi nimekuwa baba wa Israeli, Efuraimu ni muzaliwa wangu wa kwanza.
Ni yeye aliyewaongoza katika lile jangwa kubwa na la kutisha, lenye nyoka wenye sumu na nge katika inchi ile yenye kukauka isiyokuwa na maji, aliwatolea maji kutoka kwenye jiwe gumu.
Basi yule aliyekuwa akiikaa juu ya kiti cha kifalme akasema: “Angalia ninafanya vitu vyote kuwa vipya.” Kisha akaniambia: “Andika maneno haya, kwa maana ni ya kweli na ya uhakika.”