Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 43:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16-17 Zamani Yawe alifanya barabara katika bahari na kuweka njia kati ya maji mengi. Alipiga kundi la waaskari lenye nguvu, kundi la magari na farasi wa vita, waaskari na mashujaa wa vita. Aliwaangusha chini hata hawawezi kusimama tena, Aliwakomesha na kuwazimisha kama utambi wa taa. Sasa Yawe anasema hivi:

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 43:16
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Uligawanya bahari katikati mbele yao, nao wakapita katikati ya bahari, pahali pakavu. Lakini ukawatupa Wamisri waliowafuatilia kama jiwe zito ndani ya maji mengi.


Alikaripia bahari Nyekundu, ikakauka; akawapitisha humo kama katika inchi kavu.


Kishindo cha ngurumo yako kilitokea katika zoruba, umeme wako ukaangaza ulimwengu, dunia ikatikisika na kutetemeka.


Wewe ukajifanyia njia juu ya bahari; ulitembea juu ya maji yale mengi, lakini pahali ulipopita hapakuonekana.


Aligawanya bahari, akawapitisha ndani yake; aliyafanya maji yasimame kama ukuta.


Inua fimbo yako na kuielekeza juu ya bahari. Maji yatagawanyika na Waisraeli wataweza kuvuka katikati ya bahari pahali pakavu.


Lakini Waisraeli walipita katikati ya bahari pahali pakavu, kuta za maji zikiwa zimesimama upande wao wa kuume na wa kushoto.


Mukipita katika maji, mimi nitakuwa pamoja nanyi; mukipita katika mito, haitawashinda nguvu. Mukitembea katika moto, hamutaungua; ulimi wa moto hautawaunguza.


Mimi ndiye ninayeviamuru vilindi: Mukauke, nitakausha mito yenu.


Nilipokuja, kwa nini sikukuta mutu? Nilipoita mbona hamukuitikia? Mukono wangu ni mufupi hata nisiweze kuwaokoa ninyi? Sina nguvu ya kuwakomboa? Ninakausha bahari kwa kuikaripia, na mito ninaifanya kuwa jangwa; samaki wake wanakufa na kunuka kwa kukosa maji.


Wewe ndiwe uliyekausha bahari, ndiwe uliyevikausha vilindi vya maji na kufanya njia katika vilindi vya bahari, kusudi wale uliowakomboa wavuke humo.


Mimi ni Yawe, Mungu wako, ninayechafua bahari, zoruba yake ikinguruma; Yawe wa majeshi, ndilo jina langu!


Yawe, yule aliyepanga jua liangaze muchana, mwezi na nyota viangaze usiku, na anayevumisha mawimbi ndani ya bahari, yule ambaye jina lake ni Yawe wa majeshi, anasema hivi:


Malaika wa sita akamwanga kikombe chake katika muto mukubwa Furati. Maji yake yakakauka kusudi njia itengenezwe kwa ajili ya wafalme wanaotoka mashariki.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ