Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 43:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Mimi ni Mungu na nitakuwa Mungu siku zote. Hakuna anayeweza kuepuka nguvu yangu; hakuna anayeweza kupinga ninayofanya.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 43:13
33 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wewe unajua kwamba mimi sina kosa, na hakuna wa kuniokoa toka katika mikono yako.


Kama Mungu akinyamaza, nani anayeweza kumuhukumu? Kama akificha uso wake, nani anayeweza kumwona, ikiwa ni taifa au mutu mumoja?


Yeye akitwaa kitu kwa rafla, nani anayeweza kumuzuia? Nani anayeweza kumwuliza: “Unafanya nini?”


Lakini wewe unabaki sawasawa, na maisha yako hayana mwisho.


“Mufikiri vizuri jambo hili, enyi musionijali, kama sivyo nitawaangamiza, wala hakuna atakayewaokoa.


Mbele milima haijakuwa, mbele haujauumba ulimwengu, wewe ndiwe Mungu, milele na milele.


Kiti chako cha kifalme ni imara tangu zamani; wewe umekuwa mbele ya nyakati zote.


Hakuna hekima, ufahamu, wala shauri yoyote ya mutu, itakayoweza kupingana na Yawe.


Nilifanywa kwa mwanzo wa nyakati, nilikuwa niko mbele ya dunia kuanza.


Kama Yawe wa majeshi ameamua, nani atakayeweza kuvunja uamuzi wake? Kama anaunyoosha mukono wake kutoa azabu, ni nani atakayemupinga?


Nani aliyefanya yote haya yatendeke? Ni nani aliyepanga wakati wa kila tukio? Mimi Yawe nipo tangu mwanzo, mimi nitakuwa hata milele.


Nilitangaza mambo ya mwisho tangu mwanzo, tangu zamani nilitangaza mambo yatakayotukia. Kusudio langu litatimia; mimi nitatimiza nia yangu yote.


Mimi nitabaki yuleyule hata katika uzee wenu; hata katika wakati wenu wa imvi mimi nitawabeba. Nilifanya hivyo kwanza, nitafanya hivyo tena. Nitawabeba ninyi na kuwaokoa.


Ndivyo watakavyokuwa hao uliowategemea hivyo, hao uliojishugulisha nao tangu ujana wako. Watatangatanga kila mumoja njia yake; hakuna hata mumoja atakayeweza kukuokoa.


Musogee karibu nami musikie jambo hili: Tangu mwanzo mimi sikusema kwa siri, tangu mambo hayo yaanze kutendeka, nimekuwa pale. Sasa, Bwana wetu Yawe amenituma, na kunipa nguvu ya Roho wake.


Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.


Hakujua kwamba ni mimi niliyemupa ngano, divai na mafuta, niliyemujalia feza na zahabu kwa wingi, ambazo alimupelekea mungu Bali.


Maana mimi nitakuwa kama simba kwa Efuraimu, kama simba mukali kwa watu wa Yuda. Mimi mwenyewe nitawararua na kuondoka, nitawakamata na hakuna atakayewaokoa.


Hivyo Mungu atawaachilia watu wake kwa waadui, mpaka yule mwanamuke mwenye kuwa na mimba atakapozaa. Kisha wandugu zake waliobakia, watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.


Wewe si ndiwe Yawe, tangu zamani sana? Wewe ndiwe Mungu wangu, Mutakatifu wangu, usiyekufa. Ee Yawe, umewachagua Wakaldea watuhukumu! Ewe kimbilio letu, umewaimarisha kusudi watuazibu!


Nimepewa amri ya kubariki, naye amebariki wala siwezi kuigeuza.


Yesu akawajibu: “Kweli, kweli ninawaambia: mbele Abrahamu hajazaliwa, mimi nilikuwa niko.”


Mungu amefanya kila kitu kufuatana na kusudi na mapenzi yake. Yeye ametuchagua kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo, kusudi tukuwe watu wake.


Ngombe wenu watachinjwa mbele ya macho yenu lakini hamutaonja hata kipande cha nyama yao. Punda wenu watatwaliwa kwa nguvu mbele ya macho yenu wala hamutarudishiwa. Kondoo wenu watapewa waadui zenu, na hakuna mutu atakayeweza kuwasaidia.


Muone kwamba mimi ni Mungu na wala hakuna mwingine isipokuwa mimi. Mimi ninaua na kuweka uzima, ninaumiza na kuponya, na hakuna anayeweza kumwokoa yeyote toka katika mikono yangu.


Kwa Mufalme wa milele, asiyeweza kufa, asiyeonekana, Mungu peke yake, ikuwe heshima na utukufu milele na milele! Amina.


Yesu Kristo ni yule yule, jana, leo na hata milele.


Mufalme wa muji wa Yeriko akaambiwa: “Wanaume wawili Waisraeli wameingia katika muji leo usiku kwa kuipeleleza inchi.”


Bwana Mungu Mwenye Uwezo anasema: “Mimi ni Alfa na Omega.” Ni yeye anayekuwa, aliyekuwa na anayekuja.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ