Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 43:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Ninyi Waisraeli ni washuhuda wangu. –Ni ujumbe wa Yawe.– Niliwachagua mukuwe watumishi wangu, mupate kunijua na kuniamini, kwamba mimi ni Mungu. Mbele yangu hakukuwa mungu mwingine, wala hakutakuwa mungu mwingine nyuma yangu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 43:10
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Vitatoweka na kuchakaa kama nguo, lakini wewe utabaki. Utavibadilisha kama nguo, navyo vitapita.


Mufalme wa Misri akamwambia: “Kesho.” Musa akasema: “Nitafanya kama vile unavyosema, kusudi ujue kwamba hakuna yeyote anayelingana na Yawe, Mungu wetu.


Watu wataona jambo hilo, nao watatambua na kuelewa kwamba mimi Yawe nimetenda hayo, mimi Mutakatifu wa Israeli nimefanya jambo hilo.


Nani aliyefanya yote haya yatendeke? Ni nani aliyepanga wakati wa kila tukio? Mimi Yawe nipo tangu mwanzo, mimi nitakuwa hata milele.


Sikiliza ewe Israeli, mutumishi wangu, wewe, Yakobo ambaye nimekuchagua, wewe wa uzao wa Abrahamu, rafiki yangu;


Muangalie mutumishi wangu ninayemusaidia; muchaguliwa wangu ambaye moyo wangu umependezwa naye. Nimeiweka roho yangu juu yake, naye ataimarisha sheria yangu katika mataifa.


Nilitangaza yale ambayo yangetukia, kisha nikakuja na kuwakomboa. Hakuna mungu mwingine aliyetangulia kufanya hivyo, nanyi ni washuhuda wangu. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Mimi ni Yawe, wala hakuna mwingine; hakuna Mungu mwingine lakini mimi. Ninakuimarisha ingawa wewe haunijui,


kusudi watu wote, toka mashariki mpaka magaribi, wajue kwamba hakuna Mungu mwingine isipokuwa mimi tu. Mimi ni Yawe na hakuna mwingine.


Unisikilize ee taifa la Yakobo, unisikilize ee Israeli niliyekuita. Mimi ndiye. Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.


Wafalme watakushugulikia, na malkia watakutengenezea chakula. Watainama mbele yako uso mpaka chini, na kulambula mavumbi ya miguu yako. Halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe; wote wanaonitegemea hawatapata haya.


Mimi nilimufanya kuwa mukubwa na mutawala wa mataifa kusudi yeye anishuhudie kwa watu wa mataifa.


Siku hiyo, nitakutwaa wewe Zerubabeli mwana wa Saltieli, mutumishi wangu. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi! Nitakusimika utawale kwa jina langu. –Ni ujumbe wa Yawe! Wewe ndiwe niliyekuchagua. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi!


Na ninyi vilevile mutanishuhudia, kwa sababu mumekuwa pamoja nami tangu mwanzo.


Lakini hii imeandikwa kusudi mupate kuamini kwamba Yesu ni Kristo, Mwana wa Mungu, na kwa kumwamini mupate uzima katika jina lake.


Lakini mutapokea uwezo wakati Roho Mutakatifu atakaposhuka juu yenu. Nanyi mutakuwa washuhuda wangu katika Yerusalema, katika Yudea yote na Samaria na hata katika inchi zote za dunia.”


Na zaidi ya hii, sisi tumeonekana kuwa washuhuda wa uongo mbele ya Mungu, kwa sababu tumeshuhudia kuwa Mungu amemufufua Kristo, ingawa hakumufufua, ikiwa kweli wafu hawafufuki.


Muone kwamba mimi ni Mungu na wala hakuna mwingine isipokuwa mimi. Mimi ninaua na kuweka uzima, ninaumiza na kuponya, na hakuna anayeweza kumwokoa yeyote toka katika mikono yangu.


Ninyi mulijaliwa kuona mambo hayo, kusudi mupate kutambua kwamba Yawe ndiye peke yake Mungu na wala hakuna mwingine.


Basi, mukumbuke leo na kuweka ndani ya mioyo yenu, kwamba Yawe ndiye Mungu juu mbinguni na chini katika dunia. Hakuna mwingine.


Alitupilia hivi vyote, akatwaa hali ya mutumwa. Akatwaa mufano wa mutu, naye akaonekana katika hali ya kimutu.


Ni Epafra mutumishi mwenzetu mupenzi, ndiye aliyewafundisha ninyi habari zile. Yeye ni mutumishi mwaminifu wa Kristo kwa ajili yetu.


Naye Yoane alishuhudia kwamba mambo yote aliyoona yanaelekea Neno la Mungu na ukweli ulioshuhudiwa na Yesu Kristo.


na kutoka kwa Yesu Kristo. Yeye ni mushuhuda mwaminifu, naye ndiye wa kwanza aliyefufuliwa, vilevile yeye ni mukubwa wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda na ametukomboa toka katika zambi zetu kwa njia ya damu yake.


“Umwandikie malaika wa kanisa la Laodikia hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayeitwa ‘Amina’, mushuhuda mwaminifu, mwenye ukweli, na musingi wa viumbe vyote vya Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ