Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 42:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Hivi ndivyo anavyosema Yawe aliyeumba mbingu na kuzitandika kama hema, aliyeifanya dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake, anayewapa watu wanaokaa ndani yake uzima, na kuwajalia uzima wote wanaoishi ndani yake:

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 42:5
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hapo mwanzo, Mungu aliumba mbingu na dunia.


Halafu Yawe Mungu akamwumba mwanaume kwa udongo, akamupulizia ndani ya pua pumzi ya uzima, na yule mwanaume akakuwa kiumbe chenye uzima.


Uzima wa kila kiumbe, pumzi ya kila mwanadamu, viko katika mikono yake.


ninaapa kwamba kadiri ninavyoweza kupumua, roho ya Mungu ikiwa bado ndani yangu,


Roho ya Mungu iliniumba, nayo pumzi ya Mungu Mwenye Uwezo inanipa uzima.


Kama Mungu angejifikiri tu yeye mwenyewe, akiondoa pumzi yake ya uzima katika dunia,


Alitengeneza inchi juu ya vilindi vya maji. Wema wake unadumu milele.


Mbingu ziliumbwa kwa neno la Yawe, na vyote vinavyokuwa ndani yake kwa pumzi ya kinywa chake.


Miungu ya mataifa si kitu; lakini Yawe ndiye aliyeumba mbingu.


“Ee Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, unayeikaa katika kiti cha kifalme juu ya makerubi, ni wewe tu unayekuwa Mungu, unayetawala falme zote za ulimwengu. Wewe uliumba dunia na mbingu.


Ni nani anayeweza kupima maji ya bahari katika kitanga cha mukono wake, na kuzipima mbingu kwa mikono yake? Ni nani anayeweza kuutia udongo wa dunia katika kikombe; kuipima milima kwa mizani au vilima kwa kipimo cha uzito?


Dunia iliumbwa na yule anayeikaa juu ya mbingu; kutoka huko wakaaji wa dunia ni kama mapanzi! Yeye ametandika mbingu kama pazia, na kuzikunjua kama hema la kuishi ndani yake.


Muinue macho yenu juu mbinguni! Ni nani aliyeziumba nyota hizo? Ni yule anayeziongoza kama jeshi lake, anayeijua hesabu yake yote, anayeziita kila moja kwa jina lake. Kwa sababu yeye ni mwenye nguvu nyingi, hakuna hata moja inayokosekana.


Ninyi hamujui bado? Hamujapata kusikia? Yawe ndiye Mungu wa milele; yeye ndiye Muumba wa kila kitu katika dunia. Yeye haregei hata kidogo wala kuchoka. Maarifa yake hayachunguziki.


Yawe, Mukombozi wako, aliyekuumba tangu katika tumbo, anasema hivi: Mimi ndiye Yawe niliyeumba vitu vyote. Mimi peke yangu nilizitandaza mbingu, niliiumba dunia kwa nguvu yangu mwenyewe!


Ni mimi niliyeifanya dunia, na kuumba mwanadamu anayeishi humo. Mikono yangu ndiyo iliyozitandaza mbingu, na kundi lote la nyota liko kwa amri yangu.


Hivi ndivyo anavyosema Yawe aliyeumba mbingu, ndiye Mungu aliyeipa dunia umbo na kuifanya na kuiimarisha. Hakuiumba kusudi ibaki ukiwa, lakini aliipa umbo kusudi iikaliwe na viumbe vyake: Mimi ni Yawe, wala hakuna mwingine.


Kwa mukono wangu niliuweka musingi wa dunia, mimi mwenyewe nilizitandaza mbingu. Nikiziita mbingu na dunia, zinasimama haraka mbele yangu.


Maana sitaendelea kugombana wala kuwakasirikia siku zote, maana hao niliowaumba watazimia mbele yangu, nami ndiye niliyewapa pumzi yangu ya uzima.


Yawe aliiumba dunia kwa nguvu zake; kwa hekima yake alisimamisha ulimwengu imara, kwa akili yake alizitandika mbingu juu.


Ni mimi niliyeumba dunia, watu na nyama wanaokuwa ndani yake kwa uwezo wangu na kwa nguvu zangu kubwa. Nami ninaitoa kwa yeyote ninayetaka.


Ee Bwana wangu Yawe, ni wewe ambaye kwa nguvu zako nyingi na uwezo wako mukubwa, umeziumba mbingu na dunia.


Halafu, mufalme Zedekia alimwapia Yeremia kwa siri akisema: Kama vile Yawe, yule aliyetupatia uzima, anavyoishi, sitakuua wala sitakutia katika mikono ya hawa wanaotaka kukuua.


Mujue kwamba uzima wa kila mutu ni katika mikono yangu, ikiwa uzima wa muzazi na uzima wa mutoto. Yeyote anayetenda zambi, ndiye atakayekufa.


Pahali pake umejitukuza mwenyewe mbele ya Bwana wa mbinguni: umeleta vyombo vya nyumba ya Mungu ukavitumia kwa kunywea divai, wewe, wakubwa wako, wanawake wako na wahabara wako, na kuisifu miungu iliyotengenezwa na feza, zahabu, shaba, chuma, miti na mawe; miungu ambayo haioni, haisikii wala haijui jambo lolote. Lakini Mungu, ambaye uzima wako uko katika mukono wake, na njia zako ziko wazi mbele yake, haukumuheshimu!


Yawe amejenga makao yake mbinguni, nayo dunia akaifunika kwa anga; anayaita maji ya bahari, na kuyamwanga juu ya inchi kavu. Yawe, ndilo jina lake!


Ujumbe wa Yawe unaoelekea Israeli. Yawe aliyezitandaza mbingu, aliyeiweka misingi ya dunia na kumupa mwanadamu uzima anasema hivi:


Mungu aliyeumba ulimwengu na vitu vyote vinavyokuwa ndani yake, yeye anayekuwa Bwana wa mbingu na dunia, hakai ndani ya hekalu zilizojengwa na watu.


Yeye hahitaji kushugulikiwa na watu, kama vile angekuwa na lazima ya musaada fulani. Kwa maana yeye ndiye anayewapa watu wote pumzi ya uzima, pamoja na vitu vyote wanavyohitaji.


Lakini kwa siku hizi za mwisho amesema nasi kwa njia ya Mwana wake. Mungu alimuweka kuwa murizi wa vitu vyote, na ambaye kwa njia yake aliumba ulimwengu wote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ