Lakini hawa ni watu walioibwa mali yao na kunyanganywa! Wote wamenaswa katika mashimo, wamefungwa katika kifungo. Wamenyanganywa bila mutu wa kuwaokoa, wamekamatwa mateka na hakuna anayesema: Muwarudishe!
Ni nani aliyewatia Waisraeli katika mikono ya waadui zao? Nani aliyewaacha wanyanganywe mali zao? Ni Yawe ambaye tumemukosea! Wazee wetu walikataa kuzifuata njia zake, wala hawakuzitii amri zake.
Wewe, kubali tu kosa lako: kwamba umeniasi mimi Yawe, Mungu wako; kwamba chini ya kila muti wenye majani, umeonyesha mapenzi yako kwa miungu mingine, wala haukuitii sauti yangu. –Ni ujumbe wa Yawe.