Kila siku wananitafuta, wanatamani kujua njia zangu, kama vile wao ni taifa linalotenda haki, taifa lisilosahau agizo la Mungu wao. Wanataka niamue kwa haki, na kutamani kuikaa karibu na Mungu.
Basi, wanakuja kwako makundi kwa makundi na kuikaa mbele yako kama watu wangu, kusudi wasikie unachosema, lakini hawafanyi unachowaambia wafanye. Wanasema kwamba wana upendo, lakini hayo ni kusema tu; wanachotafuta kwa moyo ni faida yao tu.
Kwao, wewe umekuwa tu kama mwimbaji wa kubembeleza mwenye sauti nzuri ikiandamana na muziki safi! Wanayasikia yale unayosema, lakini hawatii hata neno moja.
hakuna hata mumoja wao ambaye amekwisha kuuona utukufu wangu na vitambulisho vyangu nilivyofanya Misri na katika jangwa kisha akazidi kunijaribu mara hizi zote bila ya kutii sauti yangu,
“Lakini mukuwe waangalifu na kufanya angalisho sana kusudi musisahau mambo yale muliyoona kwa macho yenu wenyewe, kusudi isitokee hata mara moja katika maisha yenu mambo hayo kusahaulika ndani ya mioyo yenu. Muwaelezee watoto wenu na wajukuu wenu