18 Musikilize enyi viziwi! Muangalie, enyi vipofu, mupate kuona!
Halafu Yawe akamwuliza: “Ni nani aliyeumba kinywa cha mutu? Ni nani anayemufanya mutu kuwa bubu au kiziwi? Aone au akuwe kipofu? Si mimi Yawe?
Sikio linalosikia na jicho linaloona, vyote viwili vimefanywa na Yawe.
Siku hiyo viziwi watasikia ujumbe ukisomwa katika kitabu na kutoka katika giza, vipofu wataanza kuona.
Hapo vipofu wataona tena, na viziwi watasikia tena.
Muwalete mbele watu hao, ambao wana macho lakini hawaoni, wana masikio lakini hawasikii!
Halafu Yesu akawajibu wale wajumbe: “Mwende kumwelezea Yoane mambo muliyoona na kusikia: vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanapata kusikia, wafu wanafufuliwa na Habari Njema inahubiriwa kwa wamasikini.