Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 42:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Nitawaongoza vipofu katika njia wasiyoifahamu, nitawaongoza katika njia ambazo hawazijui. Mbele yao nitaligeuza giza kuwa mwangaza, na pahali penye kuharibika patakuwa laini. Huo ndio mupango wangu wa kufanya, nami nitautimiza.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 42:16
40 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe hatawaachilia watu wake; hatawatupa hao wanaokuwa mali yake.


Kitu kilichokunjama hakiwezi kunyooshwa. Kitu kisichokuwa hakiwezi kuhesabiwa.


Mufikiri vema juu ya kazi ya Mungu. Ni nani anayeweza kunyoosha kitu Mungu alichokunja?


Njia ya watu wa haki ni yenye kunyooka; ewe Mungu mwenye haki, unasawanisha njia yao.


Siku hiyo viziwi watasikia ujumbe ukisomwa katika kitabu na kutoka katika giza, vipofu wataanza kuona.


Waliopotoka katika roho watapata maarifa na wenye kunungunika watakubali kufundishwa.


Hata hivyo, Yawe anangoja kuwasamehe, atasimama na kuwaonea huruma. Yawe ni Mungu wa haki. Heri wote wale wanaomutumainia.


Mukienda kwa upande wa kuume au kushoto, mutasikia sauti nyuma yenu ikisema: Njia ni hii; muifuate.


Macho ya wanaoona hayatapofushwa tena, masikio ya wanaosikia yatabaki wazi.


Hapo vipofu wataona tena, na viziwi watasikia tena.


Humo kutakuwa barabara kubwa, nayo itaitwa Njia Takatifu. Watu wachafu hawatapitia humo, lakini wale watu wa Mungu tu; wapumbafu hawatakanyaga ndani yake,


Kila bonde litafunikwa, kila mulima na kilima vitasawanishwa; njia zenye lukumba zitanyooshwa, nazo zenye mashimo zitalainishwa.


Wamasikini na wakosefu wakitafuta maji lakini hawayapati, wakiwa wamekauka koo kwa kiu, mimi Yawe nitawajibu; mimi Mungu wa Israeli, sitawaacha.


Yeye anawakimbiza na kupita kwa usalama; anaenda mbio bila kukanyaga chini.


Mimi nitakutangulia, na kuisawanisha milima mbele yako. Nitaivunjavunja milango ya shaba, na kuvikatakata vifungio vyake vya chuma.


Mimi ninafanya mwangaza na kuumba giza; ninaleta uheri na kusababisha hasara. Mimi Yawe ninatenda vitu hivi vyote.


Yawe, Mutakatifu wa Israeli, Mukombozi wako, anasema hivi: Mimi ndiye Yawe, Mungu wako; ninayekufundisha kwa faida yako na kukuongoza katika njia unayotakiwa kwenda.


Mara hii hamutatoka kwa haraka, wala hamutaondoka mbiombio! Maana Yawe atawatangulia, Mungu wa Israeli atawalinda nyuma yenu.


Watu wako watafundishwa nami Yawe, wana wako watapata ustawi mwingi.


mukiwapa wenye njaa chakula, mukitimiza mahitaji ya wenye kuteswa, mwangaza utawaangazia nyakati za giza, giza lenu litakuwa kama muchana.


Ninyi mutaitwa: Watu Watakatifu, Watu waliokombolewa na Yawe. Nawe Yerusalema utaitwa: Muji Mungu anaoupenda, Muji ambao Mungu hakuuacha.


Mienendo na matendo yao vitakuhakikishia kwamba hasara niliyouletea muji huo sikuileta bila sababu. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Nitaiharibu mizabibu yake na tini zake, anayosema ni malipo kutoka kwa wapenzi wake. Nitaifanya ikuwe pori, nao nyama wa pori wataikula.


Na watoto wake sitawahurumia, maana ni watoto wa uzinzi.


Huyo aliyezifanya nyota zinazoitwa Kilimia na Orioni, ambaye analigeuza giza nene kuwa muchana, na muchana kuwa usiku; yeye anayekusanya maji ya bahari na kuyamwanga juu ya inchi kavu, Yawe ndilo jina lake.


Hivi kila bonde litafunikwa. Kila mulima na kila kilima vitasawanishwa. Njia zenye lukumba zitanyooshwa, nazo njia zenye mashimo zitalainishwa.


kusudi ufungue macho yao, ukiwaongoza watoke katika giza na kuwaingiza katika mwangaza. Watatoka chini ya uwezo wa Shetani na kumugeukia Mungu, kusudi kwa njia ya kuniamini wapate kusamehewa zambi zao na kupewa urizi pamoja na watu wake watakatifu.’


Zamani muliishi katika giza, lakini sasa, kwa kuungana kwenu na Bwana, munaishi katika mwangaza. Muishi kama watoto wa mwangaza,


Musijiachilie kutawaliwa na tamaa ya mali katika maisha yenu, lakini mutoshelewe na vitu munavyokuwa navyo, kwa maana Mungu mwenyewe amesema: “Sitakusahau wala kukuachilia.”


ndivyo mutakavyojua njia ya kupita maana hamujapita huku hata kidogo. Lakini musilikaribie sana Sanduku la Agano; mukuwe kwa umbali wa kilometre moja hivi.”


Lakini ninyi ni watu wa kizazi kilichochaguliwa na Mungu na wa ukuhani wa kifalme. Ninyi ni taifa takatifu na watu wa pekee wa Mungu. Mumechaguliwa kusudi mutangaze matendo makubwa ya yule aliyewaita kutoka katika giza na kuwaingiza kwenye mwangaza wake wa ajabu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ