Isaya 42:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
11 jangwa na miji yake yote vipige kelele, vijiji vya wakaaji wa Kedari vimusifu, wakaaji wa Sela waimbe kwa shangwe; wapige kelele kutoka juu kwenye mulima.
Yawe akamwambia: “Mataifa mawili yako ndani ya tumbo lako; makabila mawili yatakayozaliwa nawe, yatatengana. Moja litakuwa lenye nguvu kuliko lingine, mukubwa atamutumikia mudogo.”
Makundi ya nyama wa inchi ya Kedari yatakusanyika kwako, utaweza kuwatumia kondoo dume wa Nebayoti; utatoa sadaka inayokubaliwa kwenye mazabahu ya Mungu, naye ataitukuza nyumba yake tukufu.
Sasa mimi nitapigana nanyi: ninyi munaoishi katika bonde, munaokaa kwenye mawe katika uwanja, ninyi munaosema: Nani atasubutu kutushambulia? Nani anayeweza kuingia katika makao yetu?
Vitisho unavyotoa na kiburi chako vimekudanganya, ewe unayekaa katika mapango ya mawe, unayeishi juu ya kilele cha mulima! Ingawa unaweka makao yako juu kama ya tai, mimi nitakuporomosha kutoka huko unakokuwa. –Ni ujumbe wa Yawe.
Simama uende kulishambulia taifa linalostarehe, taifa linaloishi kwa usalama. –Ni ujumbe wa Yawe.– Taifa hilo halina milango wala vifungio vya chuma; ni taifa ambalo liko peke yake.
Kiburi chako kimekudanganya: wewe unayekaa ndani ya mashimo chini ya mawe makubwa na makao yako yapo juu kwenye milima, hivyo unajisemesha: Nani anayeweza kunishusha chini?