Fundi anamusaidia mufuaji wa zahabu. Naye anayelainisha sanamu kwa hama, anamusaidia anayeiunga kwa misumari. Wote wanasema: Ni vizuri sana! Kisha wanaifunga kwa misumari isitikisike.
Mufuaji wa vyuma anatwaa kipande cha chuma, anakiyeyusha kwa moto na kufua sanamu. Anakipondaponda na nyundo kusudi akipatie umbo kwa mikono yake yenye nguvu. Wakati wote huo yeye anasikia njaa na kuchoka; anasikia kiu na nguvu kuregea.